LATEST POSTS

Wednesday, November 13, 2013

MTOTO HUYU AMETESEKA KWA ZIADI YA MIAKA SITA. ANAHITAJI MSAADA!

   
Na Imelda Mtema
 

WAKATI mamilioni ya watoto duniani wanafurahi kutokana na wazazi wao kuwa na uwezo wa kuwapeleka shule, sambamba na afya zao kuwa nzuri, hali ni tofauti kabisa kwa mtoto Hamisi Hashimu, mkazi wa Yombo Buza jijini Dar es Salaam ambaye kwa zaidi ya miaka sita sasa, yupo katika mateso makubwa.

Hamis mwenye umri wa miaka 12, aliyezaliwa akiwa mzima wa afya, alipata ulemavu ghafla wakati akicheza na watoto wenzake, lakini jitihada za wazazi wake kumpeleka hospitali ya CCBRT ziligonga mwamba baada ya maradhi yake ya kuvimba mguu kushindwa kutibika na hivyo kulazimika kumrudisha nyumbani ambako hakwenda tena kutibiwa.

Akizungumza kwa uchungu, kijana huyo alisema anakumbuka siku moja akiwa mdogo alikuwa anacheza na wenzake ndipo miguu yake ilipovunjika kwa zaidi ya miaka sita sasa, mguu wake unaongezeka ukubwa kutokana na kuvimba, kitu kinachomfanya ashindwe kabisa kutembea.

“Mimi mpaka sasa hivi naendelea kuteseka kwa sababu wazazi wangu hawana uwezo kabisa wa kunisaidia kuhangaikia matibabu, kila siku mguu unaendelea kuwa mkubwa,” alisema Hamis.

Lakini katika hali ya kusikitisha zaidi, licha ya ulemavu huo unaompatia maumivu makubwa, bado Hamisi hulazimika kwenda Kariakoo kwa ajili ya kuomba hela kwa wasamaria wema mwishoni mwa wiki ili aweze kujikimu yeye na familia yao ambayo ni maskini.

“Huwa ninaenda shuleni kwa msaada wa kusukumwa kwenye baiskeli, siku za Jumamosi na Jumapili ndiyo huelekea Kariakoo kwa ajili ya kuomba msaada. Huu mguu ni mkubwa sana lakini kwa vile nina shida ndiyo maana najikokota ili niweze kupata fedha ya kujikimu katika maisha yangu ya kila siku,” alisema Hamisi.   
Kama umeguswa na habari za mtoto huyu na unapenda kumsaidia, wasiliana na chumba chetu cha habari kupitia namba 0713612533.

SOURCE: GLOBAL PUBLISHERS

MTUMEEE! KUMBE DIAMOND NA PENNY NI NDUGU.

MAAJABU! Jambo zito limefichuka kuwa mastaa walio katika uhusiano wa kimapenzi, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na Penniel Mwingilwa ‘Penny’ ni ndugu, AMANI limepekua na kupata mkanda kamili.

 
Diamond na Penny katika pozi la kimahaba.
Diamond kwa sasa ndiye mwanamuziki aliye matawi ya juu zaidi kuliko yeyote kwenye Bongo Fleva, akisumbua vibaya na kibao chake cha Number One wakati Penny akiingiza mkwanja kupitia utangazaji katika kituo cha Runinga ya Dar es Salaam…

 
Na Shakoor Jongo
MAAJABU! Jambo zito limefichuka kuwa mastaa walio katika uhusiano wa kimapenzi, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na Penniel Mwingilwa ‘Penny’ ni ndugu, AMANI limepekua na kupata mkanda kamili.

 

Diamond na Penny katika pozi la kimahaba.

Diamond kwa sasa ndiye mwanamuziki aliye matawi ya juu zaidi kuliko yeyote kwenye Bongo Fleva, akisumbua vibaya na kibao chake cha Number One wakati Penny akiingiza mkwanja kupitia utangazaji katika kituo cha Runinga ya Dar es Salaam ‘DTV’.


ISHU YABUMBURUKA!
Sosi wa karibu, ndani ya familia ya Diamond alinyetisha kwamba, Diamond na Penny ni ndugu wa damu lakini jambo hilo limefahamika hivi karibuni na hivyo wanahaha namna ya kuzima aibu hiyo.
Kwa sharti la kutochorwa jina gazetini, sosi huyo alisema: “Ndugu kwenye familia wanagongana. Wanajaribu kufichaficha hili jambo, lakini inashindikana. Unajua kinacholeta shida zaidi ni kwamba Diamond na Penny watakavyokuwa baada ya uamuzi kupitishwa.”
Alisema, pamoja na ukweli huo kugundulika bila shaka kuwa ni ndugu, bado kuna ugumu wa wapenzi hao waliozama kwenye dimbwi la mahaba kisha kuvunja amri ya sita, kuachana na kubaki wakiheshimiana kama kaka na dada.
“Tatizo ni je, Diamond atakubali kumchukulia Penny kama ndugu yake? Kama atakubali na Penny naye atakuwa tayari? Wote kwa pamoja wanaonekana kama wanapingana na jambo hilo,” alisema.

UNDUGU WENYEWE UKOJE?
Akieleza aina ya unasaba wa Diamond na Penny, sosi wetu huyo alisema, bibi mzaa mama wa Diamond na bibi mzaa mama wa Penny, wamezaliwa na mama mmoja.
Hapa anafafanua: “Kwa sababu hiyo sasa, unaweza kuona kuwa, wale ni sawa tu na mtu na kaka yake. Tena wako ndani ya ukoo kabisa, sema hao mabibi, kila mmoja alikuwa na baba yake, walichangia mama tu.
“Familia imejiridhisha kabisa, halafu isitoshe imeonekana kuwa, undugu wa kuchangia mama ndiyo wa uhakika zaidi kuliko wa baba ambao mtu anaweza kubambikwa hata mtoto asiye wake. Kifupi Penny na Diamond ni ndugu. Sema ndiyo hivyo historia za wazazi wao zinashangaza mpaka basi.”
Kwa mujibu wa sosi wetu, majina ya bibi hao wanaounganisha undugu ni Khadija Said Abas (bibi yake Penny) na Tatu Omar (bibi yake Diamond), wote kwa sasa wametangulia mbele ya haki.

MAMA DIAMOND ACHEKELEA
Wakati jambo hilo likileta msuguano wa kimyakimya ndani ya familia huku wengi wakitaka undugu huo uheshimiwe na uhusiano uvunjwe kabisa, imeelezwa kuwa mama Diamond, Sanura Kassim ‘Sandra’ anafurahia undugu huo


Penny akimlisha keki mama Diamond, Sanura Kassim ‘Sandra’.
“Kinachoshangaza sasa, mama Diamond amefurahi sana na amezidisha mapenzi yake kwa Penny, ndiyo maana hataki kusikia mwanaye anakuwa na mwanamke mwingine zaidi ya Penny.
“Mwenyewe anasema, kwanza undugu siyo wa karibu sana hivyo haina madhara lakini pia anajua Diamond atampenda, kumheshimu na hatamnyanyasa kwa sababu ni sehemu ya damu ya familia yao,” sosi aliendelea kutiririka.

HAPA AMANI, KULE DIAMOND
Amani lilifanya juhudi za kumsaka Diamond katika simu zake zote za mkononi bila mafanikio, likahamia kwenye mitandao ya kijamii, likamnasa ambapo awali mahojiano yalikuwa na kigugumizi lakini baadaye mambo yalikuwa hivi;
AMANI: Mzee vipi, mbona hupatikani kwenye simu zako zote? Kuna jambo nataka kukuuliza bwana mkubwa.
DIAMOND: Niko Nigeria. Vipi, kuna nini tena?
AMANI: Kuna stori fulani... eti ni kweli bibi yake Penny mzaa mama na bibi yako wewe ni ndugu wa damu kwa maana wamezaliwa na mama mmoja?
DIAMOND: Yeah but wamechangia mama, kila mmoja na baba yake.
AMANI: Kwa hiyo Penny ni dada yako kiasili si ndiyo?
DIAMOND: Yap!
AMANI: Duh! Majanga... kwa hiyo unatembea na dada yako wa damu?
DIAMOND: Nilikuwa najua basi kaka?!
AMANI: Kwa hiyo sasa baada ya kugundua hivyo, unaachana naye au?
DIAMOND: Kama nilivyokuambia, niko Nigeria... halafu niko gym sasa hivi, nitakutafuta nikitoka.
AMANI: Sawa, naomba ujibu hili swali la mwisho. Tumesikia kuwa, mama yako anampenda sana Penny, ni kwa sababu amegundua kuwa una undugu naye?
DIAMOND: Ha! Ha! Ha! Nikitoka gym nitakupigia simu tuzungumze vizuri.
Diamond hakufanya hivyo. Hata alivyotafutwa baadaye kwenye mtandao huo, pia hakuonekana kuwa hewani.

PENNY MIKONONI MWA AMANI
Penny alipopatikana juzi Jumanne, kwa njia ya simu alielezwa ilivyo ambapo alisema: “Ni kweli Diamond ni ndugu yangu wa damu. Tumegundua tukiwa tayari tumeshakuwa wapenzi.
“Hakuna jinsi tena, sanasana naona kama mapenzi yetu ndiyo yamezidi kuimarika. Nampenda sana Diamond wangu na sababu hiyo haitoshi kututenganisha maana kama ni makosa tayari yameshatokea.”

MAMA DIAMOND
Kwa upande wake mama Diamond, baada ya kusimuliwa kila kilichofika mezani mwa Amani na kutakiwa kueleza msimamo wake alijibu kwa kifupi: “Ndiyo ni kweli unayosema, lakini kwa sasa nipo huku Kariakoo (Dar), sipo kwenye nafasi nzuri ya kuzungumza. Njoo nyumbani jioni, tuzungumze vizuri.”
Diamond na Penny wamekuwa kwenye penzi lenye kasheshe nyingi kufuatia mwanamuziki huyo kuhusishwa na wanawake wengine akiwemo aliyekuwa mpenzi wake wa zamani, Wema Isaac Sepetu.

SOURCE:GLOBAL PUBLISHERS

MAINDA AFUNGUKA: NIMETOA MIMBA YA RAY

HILI ndiyo Risasi bwana! Sikia, kama ulikuwa hujui ni kwamba msanii mkongwe katika filamu za Kibongo, Ruth Suka ‘Mainda’ ameibuka na kueleza mengi ikiwemo kutoa mimba ya mpenzi wake wa siku nyingi, Vincent Kigosi, tulia hapohapo.…


Video hapo juu ni sehemu ya mahojiano kati ya GPL na Mainda. Msikilize mwanadada huyo akifunguka!.
Stori:  Jelard Lucas
HILI ndiyo Risasi bwana! Sikia, kama ulikuwa hujui ni kwamba msanii mkongwe katika filamu za Kibongo, Ruth Suka ‘Mainda’ ameibuka na kueleza mengi ikiwemo kutoa mimba ya mpenzi wake wa siku nyingi, Vincent Kigosi, tulia hapohapo
.
Ruth Suka ‘Mainda’.

Mbali na uhusiano wao huo uliokuwa ukifanywa siri, Mainda ameeleza kwa machungu jinsi Ray alivyomtesa kwa kumchanganya na wasanii wenzake, Blandina Chagula ‘Johari’ na Chuchu Hans ambaye ni mke wa mtu.
Risasi Mchanganyiko lilipata wasaa wa kufanya naye mahojiano ‘exculusive’ kwa saa moja na dakika tano, wikiendi iliyopita, makao makuu ya gazeti hili, Mwenge – Bamaga, jijini Dar.
Hata hivyo, alisema uhusiano wao kwa sasa umevunjika rasmi huku akibainisha jinsi alivyonyooshewa vidole na watu wakiamini kwamba aliambukizwa Ukimwi na aliyekuwa mpenzi wake kabla ya Ray, marehemu Said Maulid Banda  ‘Maxi’.
Soma mwenyewe mahojiano yalivyokuwa mstari kwa mstari, neno kwa neno:

 
Vincent Kigosi 'Ray'.

Risasi: Baada ya kifo cha Maxi, Ray alijitokeza na kukutongoza au siyo?
Mainda: Hapana, nakumbuka ilikuwa Siku ya Valentine’s Day mwaka 2004...sikumbuki kama tulitongozana ama vipi lakini ilitokea tukajikuta kwenye uhusiano.
Risasi: Umedumu kwa muda gani katika uhusiano wako na Ray?
Mainda: Miaka tisa, nilimpenda sana hata yeye alikuwa akinipenda na kuniheshimu sana.
Risasi: Kwa nini mmeachana?
Mainda: Hajaniacha wala hatujaachana. Miye ndiye nimemwacha.

 
Chuchu Hans.
Risasi: Jeuri ya kumuacha Ray umeitoa wapi?
Mainda: Siyo jeuri, ni kujiamini na kujitambua tu.
Risasi: Chanzo cha kumuacha nini labda?
Mainda: Nilipojihakikishia kwamba anatoka na Chuchu Hans na Johari, nikafanya uamuzi.
Risasi: Lini ulipata uhakika huo?
Mainda: Ni hivi karibuni. Niliumia sana (analia).
Risasi: Pole sana, jikaze tafadhali. Siku zote ulikuwa hujui?
Mainda: Nilikuwa nasikia tu maneno, lakini nilipothibitisha nikaamua kukaa pembeni.
Risasi: Uhusiano wako na Ray ulifikia hatua gani?

 
Blandina Chagula ‘Johari’.

Mainda: Mwaka 2009 miye na Ray tulienda kanisani kwa ajili ya kutaka kufunga ndoa. Kwa sababu  mwenzangu ni Mkatoliki ilibidi aokoke na kunifuata kwenye wokovu ili tuweze kufunga ndoa yetu, nashangaa amebadilika tena.
Risasi: Ulibadili dini kwa ajili yake?
Mainda: Big no! (Hapana kabisa) ulikuwa ni uamuzi wangu binafsi.
Risasi: Mipango yenu ya ndoa ilikuwaje?
Mainda: Tulipanga kufanya private wedding (ndoa ya siri).
Risasi: Unauzungumziaje uhusiano wako na Ray? Namaanisha ni nini hasa ambacho hakitaweza kufutika kirahisi katika kumbukumbu zako?
Mainda: Daah! (anavuta pumzi ndefu kisha anazishusha) Nilimpenda sana Ray. Ilifikia hatua nikapata mimba yake. Mapenzi yetu yakaongezeka lakini kwa bahati mbaya ilitunga nje ya kizazi na ilinitesa sana, tena kwa kuwa ilikuwa ni mimba ya kwanza sikuwa nimejitambua mapema. Madaktari wakashauri niitoe, nikakubaliana nao.
Risasi: Ilikuwa ni mwaka gani?

Mwanadada Mainda katika pozi.

Mainda: Sikumbuki, ila ni kipindi tulipokuwa tukirekodi filamu iitwayo Johari (kwa kumbukumbu za Risasi ni mwaka 2005).
Risasi: Kuna madai kwamba wewe hukubaliki kwa mama yake Ray, ambaye anadaiwa anamkubali zaidi Johari, ni kweli?
Mainda: Siwezi kumsema vibaya yule mama, namheshimu sana lakini inawezekana kuna maneno ya uongo ambayo ameambiwa na watu.
Risasi: Kama yapi?
Mainda: Kuhusu miye kuwa na Ukimwi. Ngoja nikuambie kitu kaka’ngu, baada ya kifo cha Maxi, watu wengi walininyooshea vidole kwa kuamini kuwa Maxi amekufa kwa ugonjwa huo jambo ambalo siyo la kweli. Nakumbuka mwaka 2003, nilienda na Maxi Mwananyamala (Hospitali), alitolewa vipimo vingi (kikiwemo cha VVU), akabainika kuwa na kansa ya damu.
Akatakiwa kwenda Ocean Road (Hospitali) ambako walipendekeza akatwe mguu uliokuwa umeathirika na ugonjwa huo lakini alikataa. Alisema ni heri afe kwa ugonjwa huo kuliko kuzikwa akiwa na upungufu wa viungo mwilini mwake.
Risasi: Kuna tiba alishaanza kuitumia Ocean Road kabla ya kifo chake?
Mainda: Yeah! Alikuwa akichomwa mionzi, hadi kifo kilipomfika.
Risasi: Pole sana.
Mainda: Ahsante... ila baada ya kifo chake, watu wengi walihisi amekufa kwa Ukimwi na wakaamini nami pia ni mwathirika... hiyo hali ilinitesa sana (anaangua kilio).
Risasi: Pole sana, usilie...jikaze tafadhali.
Mainda: Kama kweli Maxi angekuwa amekufa kwa Ukimwi, Ray asingekubali kuwa na mimi kwa sababu  alikuwa rafiki yake na alishiriki kumuuguza kwa kiasi kikubwa.

Mainda katika pozi tofauti.
Risasi: Kwa hiyo unaamini kwamba mama Ray alipandikizwa sumu hiyo?
Mainda: Binafsi nilikuwa simfuatilii ila mwanaye alijitahidi kuniweka karibu na mama yake.
Risasi: Kivipi?
Mainda: Mara kadhaa Ray alikuwa akinipigia simu na kunitaka niongee na mama yake au ndugu zake, aliniweka karibu sana na familia yake.
Risasi: Umewahi kupima Ukimwi?
Mainda: Siyo mara moja, baada ya maneno hayo,  mwanzo nilipima kwa hofu kwa kuhisi labda wale madaktari wa Mwananyamala walinidanganya kwa vile nilikuwa mdogo.
Risasi: Majibu yako yanasomekaje?
Mainda: Namshukuru Mungu, nipo negative (hana uambukizo).
Risasi: Ulijisikiaje ulipogundua kuwa Ray anatembea na Johari na Chuchu?
Mainda: Awali sikujua na kila nilipomuuliza Ray alinikatalia.
Risasi: Kwa hiyo ulimwamini Ray?
Mainda: Sana, tena nilipokuwa naye alikuwa akiwapigia na kuweka loud speaker kisha kuwauliza kama walikuwa wapenzi, walikataa.
Risasi: Unawachukuliaje Johari na Chuchu?
Mainda: Kwangu nawaona wapumbavu na wasiojiamini katika mapenzi. Mfano kama Ray angenipigia simu na kuniuliza kama natembea naye, ningekubali bila ya wasiwasi. Walikuwa wakijua kama miye natembea na Ray lakini kwa nini wao walifanya mapenzi yao na Ray kuwa ya siri? Mfano Chuchu alikuwa akiniita first lady na aliniambia kuwa Ray ananipenda sana, kumbe kuna kitu alikuwa akinificha.
Risasi: Chuchu alikuwa rafiki yako?
Mainda: Hapana ila alikuwa akipenda kunipigia simu na kujiaminisha kwangu kwamba alikuwa na Ray na hakuna kibaya kitakachotokea.
Risasi: Ulijuaje kama Ray anatambea na Chuchu?
Mainda: Inasikitisha kwa kweli, kwanza Chuchu ni mke wa mtu, (jina la mume kapuni) kisha amezaa na mumewe mtoto mmoja lakini anatangaza mtoto huyo ni wa Ray. Anamuweka kwenye mitandao, unadhani baba yake wa kweli anajisikiaje?
Halafu inasemekana walipokwenda Mbeya na Bongo Muvi, Chuchu alilala chumba kimoja na Ray.
Risasi: Uliambiwa na nani?
Mainda: Kuna msanii mmoja anaitwa (jina kapuni) ambaye naye alikuwa akitembea na Chuchu, ndiye aliyeshuhudia Chuchu akiingia chumbani kwa Ray. Pia ndiye aliyemfumania Chuchu na Ray Msasani hivi karibuni.
Risasi: Inadaiwa siku Ray na Chuchu walipofumaniwa, ulikuwepo na ukapandisha mashetani, ni kweli?
Mainda: Siyo kweli, sikuwepo ila siku hiyo (anamtaja jina huyo jamaa) aliniletea simu za Chuchu ambazo zilikuwa na meseji alizokuwa akichati na Ray. Halafu Chuchu ndiye mwenye tabia ya kupandisha mashetani.
Risasi: Meseji za Ray kwa Chuchu zilikuwa zinasemaje?
Mainda: Mambo ya mapenzi tu, tangu hapo niliamini kwamba Ray alikuwa akitembea na Chuchu. Nikaamua rasmi kumuacha Ray aendelee na Chura wake!
Risasi: Kwa nini unamwita Chuchu Chura?
Mainda: Wenyewe ndivyo wanavyojiita yaani ni kifupi cha Chuchu (Chu) na Ray (Ra) badala ya RJ (Ray na Johari).
Risasi: Ray alijiteteaje kwako?
Mainda: Alidai kwamba simu yake ilikuwa ikitumika na rafiki yake mwingine ambaye ni mume wa mtu (jina tunalo) akidai kwamba ndiye aliyekuwa akitembea na Chuchu lakini si kweli.
Risasi: Kama leo hii Ray akikufuata na kukuomba radhi utakubali kurudiana naye?
Mainda: Ameshaomba radhi sana, hata Chuchu alishaniomba radhi na kudai kutorudia lakini mambo ni yaleyale.
Risasi: Hebu fafanua?
Mainda: Ninaujua msururu mrefu wa wanawake wa Ray, (akaanza kuwataja majina - wamo wanenguaji na wasanii wa filamu na wengine), mmoja kwa sasa ni mke wa mtu huyo sitakutajia jina lake.
Risasi: Jambo jingine?
Mainda: Sijui kama ulisikia, Ray alipata ajali na Chura wake hivi karibuni?



Risasi: Nilisikia!
Mainda: Hiyo nayo inatosha kuthibitisha ninachokisema. Hizi zote ni laana, tukio lingine ni lile la Johari kumfumania Ray akiwa na Chura.
Risasi: Hata hilo nililisikia na liliripotiwa, vipi kuhusu Johari?
Mainda: Johari naye alikuwa akinifuatilia nyendo zangu, kuna wakati nilivaa pete ya uchumba, alihaha kutaka kujua nimevalishwa na nani?
Risasi: Alijua Ray amekuvisha?
Mainda: Nadhani!
Risasi: Ni kweli?
Mainda: Tuyaache hayo.
Risasi: Kwa nini?
Mainda: (Akionesha msisitizo) tafadhali hilo tuliache kaka.
Risasi: Uliwahi kumsaliti Ray?
Mainda: Katika maisha yangu miye ndiye huumizwa kila siku. Baada ya kuwa na Maxi mwanaume mwingine ni Ray, sikuwahi kuwa na mwingine kabla na baada ya kuwa na uhusiano naye.
Risasi: Mwanaume gani alikuingiza katika dunia ya mapenzi?
Mainda: Aaah! Sitapenda kumtaja ilikuwa kabla sijakutana na Maxi.
Risasi: Unazungumza vizuri na Johari na Chuchu?
Mainda: Sina ugomvi nao, ila sikupenda kitendo cha kuchanganywa nao kwa mwanaume mmoja. Imeniuma sana, kwa kweli sipendi kuishi mitala.
Risasi: Unaionaje Bongo Muvi baada ya miaka mitano?
Mainda: Kwanza naomba Mungu aiangamize... unafiki mwingi sana. Kuna siku nilimuuliza Ray kama yeye ndiye mwenyekiti anafanya uchafu kama huu, anaweza kumkemea msanii mwingine? Hakunijibu kitu. Mengi mabaya yanayosemwa kuhusu Bongo Muvi  ni ya kweli, tena uongozi umeoza kuanzia juu mpaka chini.
Risasi: Baada ya kuachana na Ray una mwanaume mwingine?
Mainda: Wengi wamenipigia simu kunitongoza nikawachomolea wakiwemo wasanii waliokuwa wakijua uhusiano wangu na Ray.
Risasi: Kwa nini?
Mainda: Miye huwa sitongozwi kwenye simu.
Risasi: Unatongozwaje?
Mainda: (kicheko), sikia ninaye mtu wangu lakini hatujafikia hatua ya kufanya mapenzi, tunachunguzana ili kujuana tabia kwanza.
Risasi: Ni msanii wa filamu au?
Mainda: Siyo msanii, ni mtu anayejiheshimu.
Risasi: Mara yako ya mwisho kufanya mapenzi ilikuwa lini?
Mainda: Siku chache baada ya msiba wa Albert Mangweah (msanii wa Bongo Fleva).
Risasi: Unaamini iko siku utaolewa?
Mainda: Yeah! Tena nitajifungua watoto.
Risasi: Kitu gani ambacho huwezi kukisahau maishani mwako?
Mainda: Kifo cha Kanumba na marehemu Maxi  (anaangua kilio…) vifo vyao viliniuma sana na vimeshindwa kuondoka akilini mwangu kirahisi.
Risasi: Ahsante sana kwa ushirikiano wako Mainda. Karibu tena Global Publishers.

 
Mainda.

Mainda: Nashukuru sana lakini nasema hivi; kama  Ray, Johari na Chuchu watakanusha haya niliyoyasema, nipo tayari nikutanishwe nao tena hapahapa ofisini kwenu nitazungumza mbele yao. Naahidi nitaongea mengi zaidi.
Risasi: Sawa, nashukuru sana Mainda.
Mainda: Nanyi pia… ndiyo maana nayapenda magazeti yenu.
Risasi: Kwa nini unasema hivyo?
Mainda: (Kicheko).

SOURCE: GLOBAL PUBLISHERS

Tuesday, November 12, 2013

MALAWI: MAN ARRESTED FOR ATTEMPTING TO SELL HIS UNCLE

Nkhotakota — 19-year-old man Mateyo Chimphoyo is in police custody at Nkhotakota Police Station for attempting to offer on sale his uncle to a businessman in Nkhotakota district.

Nkhotakota Police Spokesperson Kaitano Lubrino said according to Maxwell Malema, 40, who hails from Matapira Village in the area of Traditional Authority Mazengera in Lilongwe, he was approached by the suspect during the afternoon hours of November 7, 2013 with the offer.
"Malema who works at Kandikole maize mill at Bzyobzyo Trading Centre in Nkhotakota said when he attended to him, the suspect urged him to go to a secret place for a discussion.
"There, Malema learnt that the suspect was offering for sale his uncle, Sainani Levison, at a price of MK 1.5 million," he said.
Lubrino said Malema was annoyed to hear this story and he wanted Chimphoyo get arrested.
"Malema then persuaded Chimphoyo to leave his bicycle behind and come back again. While away, Malema informed members of community policing from the area and Benga Police Unit.
"The suspect came again on November 9, 2013 where he got arrested at the maize mill," Lubrino said.
The police publicist said the suspect has told police that he was indeed trying to sell his uncle so that he could solve some of his financial problems.
Meanwhile, the police have opened a case of conduct likely to cause bleach of peace, which is contrary to section 181 of the Penal Code. Chimphoyo will appear before Nkhotakota Magistrate Court soon to answer the charges.

SOURCE: ALL AFRICANEWS

CHADEMA: HATUHUSIKI MADAI YA ZITTO

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimesema Ofisi ya Katibu Mkuu wa chama hicho imepokea barua iliyoandikwa na Naibu Katibu Mkuu, Bw. Zitto Kabwe.
Barua hiyo, inamtaka Katibu Mkuu wa chama hicho, Dkt. Wilbrod Slaa athibitishe madai ya ripoti inayosema“Taarifa ya Siri ya CHADEMA”iliyosambazwa katika mitandao mba limbali ya kijamii.
Taarifa hiyo inadai kuchunguza mwenendo wa Bw.Kabwe tangu mwaka 2008-2010 na kubaini amepokea fedha kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuivuruga CHADEMA.
Akizungumza na Majira jana, Ofisa Habari wa CHADEMA,Tumaini Makene,alise ma barua aliyoiandika Bw. Kabwe itafanyiwa kazi kwa mu jibu wa taratibu, kanuni za katiba ya chama.
“Chama chetu kinaongozwa na vikao hivyo barua yake itafanyiwa kazi...CHADEMA h aiendeshwi na taarifa za magazetin i au mitandaoni,”alisema Bw. Makene.
Aliongeza kuwa,si mara ya kwanza makundi yasiyojulikana kusambaza taar ifa za kutaka kumchafua Bw. Kabwe k upitia mitandao hiyo ambapo Ofisi ya Habari,ilishughulikia suala hil o na kuhakikisha taarifa hizo zinaondolewa.
“Hivi sasa ni mara ya pili, Bw. Kabwe anali fahamu hilo hivyo CHADEMA hakihusiki, lakini kitashughulikia suala hili kupitia vikao ili kupata majibu sahihi,” alisisitiza Bw.Makene.
Katika taarifa yake aliyoitoa juzi kwa vyombo vya habari, Bw.Kabwe alisema taar ifa hizo zimesambazwa katika mitandao ya kijamii hiv yo alimtaka Dkt.Slaa, athibitishe kinachoitwa“Ta arifa ya Siri ya CHADEMA”,kama ni taa rifa ya chama au kiikanushe ili kumpa fursa ya kuchukua hatua za kisheria dhidi ya waandishi wa taarifa hiyo.
Hata hivyo, Bw. Kabwe ambaye pia ni Mbunge w a Kigoma Kaskazini,aliziita taarifa hizo za kutunga zilizojaa uongo wa kiwango cha kutisha hali ambayo imemfedhehesha, kumsikitisha na kumkasirisha.
Alisema taarifa hizo ziliibuliwa katika kipindi am bacho alikuwa safarini kutetea haki za Watanza nia na Afrika ambao utajiri wao wa rasilimal i unafaidiwa na watu wachache waliohifadhi fedha katika akaunti nje ya nchi.

CHADEMA: HATUHUSIKI MADAI YA ZITTO

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimesema Ofisi ya Katibu Mkuu wa chama hicho imepokea barua iliyoandikwa na Naibu Katibu Mkuu, Bw. Zitto Kabwe.
Barua hiyo, inamtaka Katibu Mkuu wa chama hicho, Dkt. Wilbrod Slaa athibitishe madai ya ripoti inayosema“Taarifa ya Siri ya CHADEMA”iliyosambazwa katika mitandao mba limbali ya kijamii.
Taarifa hiyo inadai kuchunguza mwenendo wa Bw.Kabwe tangu mwaka 2008-2010 na kubaini amepokea fedha kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuivuruga CHADEMA.
Akizungumza na Majira jana, Ofisa Habari wa CHADEMA,Tumaini Makene,alise ma barua aliyoiandika Bw. Kabwe itafanyiwa kazi kwa mu jibu wa taratibu, kanuni za katiba ya chama.
“Chama chetu kinaongozwa na vikao hivyo barua yake itafanyiwa kazi...CHADEMA h aiendeshwi na taarifa za magazetin i au mitandaoni,”alisema Bw. Makene.
Aliongeza kuwa,si mara ya kwanza makundi yasiyojulikana kusambaza taar ifa za kutaka kumchafua Bw. Kabwe k upitia mitandao hiyo ambapo Ofisi ya Habari,ilishughulikia suala hil o na kuhakikisha taarifa hizo zinaondolewa.
“Hivi sasa ni mara ya pili, Bw. Kabwe anali fahamu hilo hivyo CHADEMA hakihusiki, lakini kitashughulikia suala hili kupitia vikao ili kupata majibu sahihi,” alisisitiza Bw.Makene.
Katika taarifa yake aliyoitoa juzi kwa vyombo vya habari, Bw.Kabwe alisema taar ifa hizo zimesambazwa katika mitandao ya kijamii hiv yo alimtaka Dkt.Slaa, athibitishe kinachoitwa“Ta arifa ya Siri ya CHADEMA”,kama ni taa rifa ya chama au kiikanushe ili kumpa fursa ya kuchukua hatua za kisheria dhidi ya waandishi wa taarifa hiyo.
Hata hivyo, Bw. Kabwe ambaye pia ni Mbunge w a Kigoma Kaskazini,aliziita taarifa hizo za kutunga zilizojaa uongo wa kiwango cha kutisha hali ambayo imemfedhehesha, kumsikitisha na kumkasirisha.
Alisema taarifa hizo ziliibuliwa katika kipindi am bacho alikuwa safarini kutetea haki za Watanza nia na Afrika ambao utajiri wao wa rasilimal i unafaidiwa na watu wachache waliohifadhi fedha katika akaunti nje ya nchi.

WAZIRI KENYA ASIFIA HOTUBA YA KIKWETE

Wizara ya Mambo ya Nje nchini Kenya, imesema bila Tanzania, hakuna Jumuiya ya Afrika Mashariki na bila Afrika Mashariki hakuna Tanzania.
Waziri wa Wizara hiyo, Amina Mohamed, aliyasema hayo Dar es Salaam jana wakati akizungumza na waandishi wa habari na kusisitiza kuwa, jambo lililomsukuma kufika Tanzania ni kuunga mkono hotuba ya Rais Jakaya Kikwete, aliyoitoa bungeni mjini Dodoma, Novemba 7 mwaka huu.
Katika hotuba yake, Rais Kikwete alisema Tanzania haiwezi kujitoa katika jumuiya hiyo au kuwa chanzo cha kuvunjika kwake.
Mohamed alisema amefikisha salama za nchi yake kwa Tanzania kutokana na hatua yake ya kutokuwa tayari kujitoa kwenye jumuiya hiyo kama ilivyodhaniwa awali.
"Tanzania na Kenya zimejiunga na jumuiya hii kwa muda mrefu na zina mafanikio mengi hivyo haziwezi kutengana hata kidogo," alisema Mohamed.
Aliongeza kuwa, Kenya inaamini nchi hizo zitaendelea kuijenga Afrika Mashariki kwa nguvu zote. "Nimetumwa na Rais Uhuru Kenyatta kuja kutoa ujumbe huu ambao ni wakati mwafaka wa kuimarisha zaidi uhusiano.
"Tulikuwa na wasiwasi wa Tanzania kujitoa katika jumuiya kutokana na hali iliyojitokeza kwa baadhi ya nchi kuendesha mikutano yao bila kuishirikisha pamoja na Burundi.
" H a k u n a a n a y e w e z a kuitenganisha Tanzania na Kenya kwani zimejenga uhusiano wa karibu kijamii na kiuchumi," alisema Mohamed.
Aliiomba Tanzania kuisaidia Kenya ili kusukuma ombi lao la kutaka kesi inayomkabili Rais Kenyatta ihairishwe kwa mwaka mmoja ili kumpa fursa ya kutekeleza majukumu yake ya kitaifa.
Kwa upande wake, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Bernard Membe, alisema Serikali yake imefurahi kuona Kenya ni nchi ya kwanza kutoa pongezi zake ili kuinusuru jumuia hiyo.
"Hili ni jambo la busara linalopaswa kupongezwa , Tanzania itaendelea kushirikiana na Kenya katika masuala mbalimbali likiwemo la kutaka kesi inayomkabili Rais Kenyatta katika Mahakama ya ICC, iahirishwe mwaka mmoja," alisema.
 
SOURCE: MAJIRA

NITAMNG'OA SPIKA MAKINDA - MBUNGE

Mbunge wa Nzega mkoani Tabora, Dkt. Hamisi Kig wangalla ,amesema bado ana dhamira ya kuwasi lisha hoja ya kumng’ oa madarakani Spika wa B unge, Bi.Anne Makinda.
Alisema uvumi ulioenea kuwa hoja yake imeondolewa kwa agizo la Chama Cha Mapinduzi (CCM), hauna ukweli.
Dkt. Kigwangalla aliyasema hayo mwishoni mwa wiki katika mkutano wa hadhara u lioshirikisha wakazi wa jimbo hilo na vitongoji vya ke uliofanyika katika Uwanja wa Parking.
Katika mkutano huo, Dkt. Kigwangalla aliulizwa swali na mkazi wa jimbo hilo kama kweli ana ubavu wa kumng’oa Bi.Makinda, anayetoka na na chama chake.
“Mheshimiwa mbunge,naomba utu thibitishie kama una uwezo wa kumng’oa Spika wa Bunge (Makinda), kama ulivyotangaza dhamira ya kuw asilisha hoja binafsi bungeni ili bunge liweze kumng’oa.
“Kwa jinsi tunavyofahamu utaratibu ndan i ya CCM, huna ubavu wa kufanya hivyo , ina onesha ulikuwa ukijifurahisha tu,”alihoji mwananchi huyo.
Mwananchi huyo aliongeza kuwa, kwa kawaida CCM ina utaratibu wa kuzuia hatua mbalimbali zinazotaka kuchukuliwa na wanachama wake hivyo alimshauri Dkt.Kigwangalla, aacha ne na hoja hiyo kwani hana ubavu wa kumng’oa Bi.Makinda.
Akijibu swali hilo,Dkt. Kigwangalla alisema,si kw eli kwamba CCM ina utaratibu wa kuondoa kin yemela hoja ambazo haikubaliani nazo ambapo suala la kutaka kumng’oa Bi. Makinda lipo ndani ya uwezo wake na kufafanua kuwa, ho ja hiyo haijaondolewa na hivi sasa ipo katika hatua za mwisho ili iweze kufikishwa bungeni.
“Kwa hili la kumng’oa Spika wa Bunge,niwaele ze wazi kuwa si kweli linaweza kunishinda... hoja imewasilishwa na Bi. Makin da atang’oka kama nikiamua kuendelea nayo kwa sababu tayari hoja nimeiwasilisha na nimekidhi masharti yote.
“Hivi tunavyoongea, hoja yangu tayari imeto ka hatua ya kwanza na kukidhi vigezo vyote sasa inaenda hatua ya pili ambayo Kamati ya Bunge y a Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge,itaamua hoja yangu iingizwe bungeni au isiingizwe,”alisema .
Aliongeza kuwa,baada ya hapo utafuata mcha kato wa mwisho ambao ni hoja hiyo kufikishwa bungeni na yeye kuiwasilisha rasmi mbele y a Bunge ili kufanyiwa uamuzi na wabunge wote kwa kupiga kura na kama atashinda au kushind wa,hilo ni jambo lingine.
Dkt.Kigwangalla alisema uamuzi wa kuo ndoka au kutoondoka kwa Spika, kutategeme au amuzi wa wabunge wenzake na kusisitiza kuwa , CCM haiwezi kuzuia hoja hiyo bila ya kupatiwa uamuzi na wabunge wote.
Akijibu swali ambalo lilihusiana na fedha za ushuru wa huduma zilizotolewa na Mgodi wa Dhahabu wa Resolute, ulioko wilayani humo, Dkt. Kigwangalla alisema fedha hizo sh.bilioni2.340,zililipwa na mgodi huo na s asa zimehifadhiwa katika akaunti maalumu ili baadaye zitumike kama mtaji wa kuanzishia Benki ya Maendeleo ya Wananchi wa Nzega.
“Fedha hizi tulizipigania kwa kiasi kikubwa hadi kuandamana lakini tulifanikiwa kuzipata, niwathibitishie zipo salama katika akaunti maalumu tuliyoianzisha ili baadaye ziweze kuanzisha Benki yetu ya Maendeleo ambayo itaweza kutupa mikopo ya kuendesha shughuli zetu,”alisema .
Alisema lengo lake ni kuhakikisha fedha hizo zinatumika vizuri ili kuwasaidia wananchi w a Nzega kubadilisha maisha yao ambapo watu watahamasishwa kujiunga katika ushirika au SACCOS ili waweze kupewa mikopo p ia zitatumika kununulia mitambo ya kutengeneza barabara na uchimbaji visima vya maji.
Gazeti moja linalotoka kila siku (si Majira), liliandika habari inayosema Dkt. Kigwangalla anadai Bi. Makinda amekiuka kanuni kwa kuidhinisha malipo ya sh. 430,000 kama posho kwa wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Bajeti, tofauti na wajumbe wa kamati nyingine ambao malipo yao ni sh. 180,000 kwa siku.
Hoja hiyo ilipingwa vikali na baadhi ya wabunge akiwemo Mbunge wa Tabora Mjini, Bw. Ismail Aden Rage (CCM) na Mbunge wa Kigoma Kusini, Bw. David Kafulila (NCCR-Mageuzi) ambao walidai hawaoni sababu ya kumuondoa Bi. Makinda madarakani.
Bw. Kafulila alisema hilo ni suala la wana-CCM, kwani Bi. Makinda aking’olewa madarakani, mtu ambaye ataziba pengo lake hawezi kutoka upinzani. Hoja hiyo ya Dkt. Kigwangalla iliibua mjadala kwa baadhi ya wabunge na wengine kukataa kusaini karatasi ambayo walipelekewa ili kuunga mkono.
Mbunge wa Ludewa, mkoani Njombe, Bw. Deo Filikunjombe, alisema hoja ya Dkt. Kigwangalla imejengwa katika msingi hafifu isiyozingatia masilahi mapana ya nchi na mtazamo finyu.
 
SOURCE: MAJIRA

WATU TISA WANASHIKIILIWA NA JESHI LA POLISI WANAOSHUKIWA KUHUSIKA KATIKA TUKIO LA DKT SENGONDO MVUNGI

Jeshi la Polisi nchini, linawashikilia watuhumiwa tisa wanaoshukiwa kumvamia, kumjeruhi na kuiba vitu mbalimbali vya Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama cha NCCR-Mageuzi, Dkt.Sengondo Mvungi.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Sa laam jana, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dkt. Emmanuel Nchimbi,alis ema kukamatwa kwa watuhumiwa hao, kumechangiwa na ushirikiano uliotolewa na familia ya Dkt. Mvungi.
Alisema watuhumiwa hao wamekamatwa jijini Dar es Salaam kwa nyakati tofauti ambapo awali walikamatwa sita lakini majina yao yalifichwa ili kutovuruga upelelezi.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna Suleiman Kova,am baye alikuwepo katika mkutano huo, waliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Msigwa Mpopela (30) ,Shabago Magozi na Hamadi Ally, jina maarufu‘Hatibu’.
Wengine ni Zakaria Raphael(dereva wa bodaboda), Mmanda Saluwa,Juma Hamisi,Longisho Semeriko(muuza ugolo), Paul Jeirosi na mwingine aliyemtaja kwa jina moja la Kilimimazoka,ambao wote ni wakazi wa Dar es Salaam
“Watuhumiwa hawa walikutwa na mapanga, kigoda ambavyo vimethibitika kuwa vilitumika katika tukio hilo, pia walikutwa na simu ya mkononi mali ya Dkt. Mvungi,”alisema.
Kamishna Kova alisema, katika mahojian o ya awali na watuhumiwa, walikiri kuhusika na tukio hilo na ushahidi umekamilika kwa asilimia 80.
“Watuhumiwa wote wamekiri kosa hivyo tunaka milisha upelelezi ili wafikishwe mahakamani mara moja,”alisema.
Dkt.Mvungi alivamiwa, kujeruhiwa na watu wanaodhaniwa kuwa majambazi us iku wa kuamkia Novemba 3mwaka huu , nyumbani kwake Kibamba, Dar es Salaam.
Hivi sasa,Dkt. Mvungi anaendelea na matibabu katika Hospitali ya Milpark, nchini Afrika Kusini na hali yake inaendelea kuimarika .
Akizungumzia suala la kuwakamata wahamiaji haramu, Dkt.Nchimbi alisema mpango wa lio nao ni kuweka Ofisa mmoja wa Polisi kilaTarafa nchini aweze kusaidiana na Polisi Jamii pamoja na wananchi kuwabaini watu hao.
 
SOURCE: MAJIRA

Saturday, October 26, 2013

WADAU WABARIKI NDOA YA WEMA SEPETU, DIAMOND

Wadau na mashabiki wa mastaa wawili nchini, Wema Sepetu wa Bongo Movie na Nasibu Abdul ‘Diamond’ wa muziki wa kizazi kipya, wamebariki ndoa ya wapenzi hao kwa kusema kuwa ni watu wanaoendana na kutegemeana kwa kiasi kikubwa.

 
Mwanzoni mwa wiki hii, Wema na Diamond walitupia katika kurasa zao za mitandao ya kijamii picha zao, ambazo zinaonekana zilipigwa eneo moja kwa simu moja na hivyo kuwapa wakati mzuri mashabiki wao ambao walionekana kupendezwa na uhusiano wao na kupendekeza waoane.
“Hii ndiyo couple bomba zaidi ya wasanii Bongo, kwa nini msioane? Mnapendeza sana jamani, ebu Diamond Platnumz achana na Penny bwana, huendani naye kwanza kuna mambo ya dini na nini…,” aliandika shabiki mmoja.
 
Mwingine aliandika: “Nadhani Penny angejiweka tu pembeni awaache hawa wawili, ni mastaa kwa fani zao, yeye angeendelea tu na kazi yake ya utangazaji. Kwanza kwake ni maumivu tu kuwa na msanii ambaye ana shughuli nyingi za kisanii, bora wale wenyewe wanajuana.”
Ingawa kwa muda mrefu Diamond amekuwa akikanusha kurudiana na Wema, hivi karibuni picha zao zilivuja katika mitandao ya kijamii wakiwa China wakila bata na alipoulizwa, ‘alizuga’ eti walikuwa wakitengeneza filamu.
Hata hivyo, uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa, wadau wengi wanaamini Wema na Diamond wanapendana kwa dhati hivyo wakapendekeza wafunge ndoa na kuyaacha maisha mengine yaendelee kuwepo kuliko kuachana kisha kurudiana mara kwa mara.

Friday, October 25, 2013

NI HUZUNI NA KUSIKITISHA: YULE MTOTO AMBAYE NDUGU ZAKE WALITAKA AUWAWE, AMEFARIKI DUNIA



INAUMA SANA! Yule mtoto ambaye aliripotiwa kuwa ndugu wanataka auawe wiki iliyopita, Mwajuma Haji (16), amefariki dunia katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar.

Mwanyuma alikuwa na ugonjwa wa kusinyaa na vipimo vya madaktari havikuonesha ugonjwa uliokuwa ukimsumbua, ingawa viungo vyake vyote vilikuwa vimesinyaa na kujikunja tangu alipozaliwa. Kutokana na tatizo hilo, baadhi ya ndugu walifikia hatua ya kutaka auawe kwa walichodai alikuwa mzigo kwa familia.
Akizungumza na mwandishi wetu kwenye mazishi ya mtoto huyo kijijini kwao Kimange, Wilaya ya Bagamoyo, Tatu alisema mwanaye alizidiwa kwa siku tatu mfululizo huku akiwa anapumulia mashine kabla mauti hayajamkuta. Alisema madaktari walijitahidi kwa hali na mali kuokoa maisha yake lakini ilishindikana kwani alikuwa akipumua kwa shida. “Mwanangu ameteseka sana dakika za mwisho kwani kwa siku tatu mfulululizo alikuwa akipumulia gesi tu mpaka Mungu alipomchukua,” alisema mama huyo. Katika mazishi ya mtoto huyo, waliokuwa karibu na mama Mwajuma ni majirani zake baada ya ndugu kuingia mitini.

Majirani wa karibu na mama Mwajuma walisema kuwa wanasikitishwa na tabia za ndugu zake waliosusia msiba huo na kudai ndiyo tabia yao kwani kipindi Mwajuma alipokuwa hai walikuwa hawamjali hata walipomkuta akinyeshewa mvua hawakumuingiza ndani hadi mama yake alipofika. “Tabia za ndugu wa mama Mwajuma hazijaanza leo kwani walikuwa wakimtenga sana mtoto huyo kwa kuwa hata walipomkuta ananyeshewa na mvua walikuwa wakimuacha hadi mama yake arudi,” alisema jirani mmoja ambaye hakupenda kutaja jina lake.

Chanzo: Amani

WAFUGAJI WA KIJIJI CHA LUMBE WALALAMIKIA FAINI YA N'GOMBE WANAYOTOZWA

WAKAZI wa Kijiji cha Lumbe, Kata ya Ukumbisiganga, wilayani Kaliua Mkoani Tabora, wamelalamikia faini ya sh 180,000 wanayotozwa kwa kila ng’ombe anayeingia katika hifadhi ya taifa na kusema faini hiyo haiwatendei haki.
 
Walitoa kauli hiyo hivi karibuni mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Fatma Mwassa, aliyetaka kujua kero zinazowakabili wafugaji wa kata hizo.
Akizungumza kwa niaba ya wafugaji wenzake, Gunze Pamagi, alisema hivi karibuni baada ya ng’ombe wao zaidi ya 5,000 kuingia kwa bahati mbaya katika hifadhi ya taifa, walikamatwa na kila ng’ombe mmoja alitozwa sh 180,000, badala ya sh 30,000.
 
Walisema hatua hiyo imewashangaza hata kufikia mahali wanahisi watu wa Maliasili hulazimisha kutaifisha mifugo yao kwa nguvu kwa ajili ya kujipatia fedha kutoka kwa wafugaji.
 
“Ni kweli mifugo yetu ilikamatwa katika hifadi ya taifa na baada ya hapo sisi tuko tayari kulipia faini hiyo lakini tunakatishwa tamaa na faini ya sh 180,000, hapa tunaona kama tunaibiwa,” alisema Pamagi.
 
Akijibu malalamiko hayo, Mwassa alisema licha ya kujionea hali hiyo, wafugaji wanapaswa kutambua kuwa zoezi linaloendelea ni la kitaifa na si la mkoa.
Alisema atakachofanya ni kumuomba waziri mwenye dhamana ili wafugaji waweze kulipa faini sitahiki.
 
Sina uamuzi mwingine kwa sasa mpaka niwasiliane na waziri mwenye dhamana ili mlipe faini stahiki, ila tambueni serikali inajua changamoto mnazokabiliana nazo,” alisema Mwassa.
 
Chanzo: Tanzania Daima

TATHMINI: HAWA NDIO MARAIS WANAOLIPWA PESA NYINGI ZAIDI DUNIANI




Rais wa Marekani analipwa Dola 400,000 (Sh 640 milioni) kwa mwaka, sawa na Sh 53.3 milioni kwa mwezi. Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma analipwa Randi 2 ,917 038 sawa na zaidi ya Sh400 milioni za Kitanzania kwa mwaka, Rais wa Ufaransa, Francois Hollande Sh475 milioni, Waziri Mkuu wa Uingereza, David Cameron Sh338 milioni, Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya Sh277 milioni na Rais wa Namibia, Hifikepunye Pohamba Sh226 milioni kwa mwaka. Wengine na malipo wanayopata kwa mwaka ni Marais wa Urusi, Vladimir Putin, Sh174 milioni,
Ellen Johnson Sirleaf wa Liberia Sh137 milioni,Michael Satta wa Zambia, Sh126 milioni, Rais wa Angola, Jose dos Santos Sh91 milioni, Rais wa Lesotho, Profesa Pakalitha Mosisili Sh88 milioni, Armando Guebuza wa Msumbiji, Sh84 milioni na Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Xi Jinping Sh60 milioni. Wengine ni Rais wa India, Pranab Mukherjee Sh49 milioni, Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe Sh27 milioni,Naibu Rais wa Afrika Kusini, Kgalema Mothlanthe Sh331 milioni,
Waziri Mkuu wa Namibia, Nahas Angula Sh160 milioni.

Ok kumbe Mshahara wa Rais wa bongo bado ni mdogo sana kulinganisha na mishahara ya Marais wenzake hapa Africa na Duniani, Mheshimiwa Zitto my hero kwenye hili hakumtendea haki Rais wetu alipotoa hadharani Mshahara wa Rais wetu ambayo nia na madhumuni yake ilikuwa kuonyesha kwamba analipwa mahela mengi sana, alitakiwa kutuonyesha pia na mishahara ya Marais wengine na vipato vya Taifa pia, kwa sababu as a nation tuna pato kubwa sana kuliko nchi nyingi zingine ambazo Marais wao wanalipwa mahela ya ajabu kulinganisha na Rais wa bongo.

Pia ifahamike wazi kwamba hata leo Rais wa Jamhuri akitokea Chadema, bado mshahara wake utakuwa ni huo huo unless akigoma na kutaka upunguzwe, kitu ambacho historia ya chama hicho na Mishahara au posho za Taifa haiko kabisa upande wao, kuna wakati walidai posho ya wabunge ni kubwa sana lakini mpaka leo hatujasikia wakiomba kupunguziwa, walilalamika kuhusu hela za magari ya wabunge lakini mpaka leo hawajagomea kupokea hela hizo, Mwenyekiti wao alilalamikia magari ya kifahari ya wabunge na yeye mpaka leo anatumia gari hilo hilo alilolalamikia!
 
-Wiliam Malecela

TATHMINI: HAWA NDIO MARAIS WANAOLIPWA PESA NYINGI ZAIDI DUNIANI


 
Rais wa Marekani analipwa Dola 400,000 (Sh 640 milioni) kwa mwaka, sawa na Sh 53.3 milioni kwa mwezi. Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma analipwa Randi 2 ,917 038 sawa na zaidi ya Sh400 milioni za Kitanzania kwa mwaka, Rais wa Ufaransa, Francois Hollande Sh475 milioni, Waziri Mkuu wa Uingereza, David Cameron Sh338 milioni, Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya Sh277 milioni na Rais wa Namibia, Hifikepunye Pohamba Sh226 milioni kwa mwaka. Wengine na malipo wanayopata kwa mwaka ni Marais wa Urusi, Vladimir Putin, Sh174 milioni,
Ellen Johnson Sirleaf wa Liberia Sh137 milioni,Michael Satta wa Zambia, Sh126 milioni, Rais wa Angola, Jose dos Santos Sh91 milioni, Rais wa Lesotho, Profesa Pakalitha Mosisili Sh88 milioni, Armando Guebuza wa Msumbiji, Sh84 milioni na Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Xi Jinping Sh60 milioni. Wengine ni Rais wa India, Pranab Mukherjee Sh49 milioni, Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe Sh27 milioni,Naibu Rais wa Afrika Kusini, Kgalema Mothlanthe Sh331 milioni,
Waziri Mkuu wa Namibia, Nahas Angula Sh160 milioni.

Ok kumbe Mshahara wa Rais wa bongo bado ni mdogo sana kulinganisha na mishahara ya Marais wenzake hapa Africa na Duniani, Mheshimiwa Zitto my hero kwenye hili hakumtendea haki Rais wetu alipotoa hadharani Mshahara wa Rais wetu ambayo nia na madhumuni yake ilikuwa kuonyesha kwamba analipwa mahela mengi sana, alitakiwa kutuonyesha pia na mishahara ya Marais wengine na vipato vya Taifa pia, kwa sababu as a nation tuna pato kubwa sana kuliko nchi nyingi zingine ambazo Marais wao wanalipwa mahela ya ajabu kulinganisha na Rais wa bongo.

Pia ifahamike wazi kwamba hata leo Rais wa Jamhuri akitokea Chadema, bado mshahara wake utakuwa ni huo huo unless akigoma na kutaka upunguzwe, kitu ambacho historia ya chama hicho na Mishahara au posho za Taifa haiko kabisa upande wao, kuna wakati walidai posho ya wabunge ni kubwa sana lakini mpaka leo hatujasikia wakiomba kupunguziwa, walilalamika kuhusu hela za magari ya wabunge lakini mpaka leo hawajagomea kupokea hela hizo, Mwenyekiti wao alilalamikia magari ya kifahari ya wabunge na yeye mpaka leo anatumia gari hilo hilo alilolalamikia!
 
-Wiliam Malecela

KAMATI YA HESABU ZA SERIKALI (LAAC) YAKATAA TAARIFA YA HESABU YA HALMASHAURI YA WILAYA YA NAMTUMBO.

MWENYEKITI wa Kamati ya Hesabu za Serikali (LAAC), Rajab Mohammed Mbarouk, amemtaka Mwenyekiti wa Halmashauri ya Namtumbo mkoani Ruvuma kutekeleza majukumu yake ipasavyo na kuacha kukidhoofisha Chama.

Pia, kamati hiyo imekataa taarifa ya hesabu ya halmashauri hiyo na kuiagiza kuifanyia marekebisho na kuirudisha tena mbele ya kamati Desemba mwaka huu.
Amesema kitendo cha kutosimamia fedha za maendeleo ya wanawake na vijana kinadhalilisha Chama chake (CCM) na kuhujumu jitihada za serikali.
Aliyasema hayo jana katika Ofisi Ndogo ya Bunge, Dar es Salaam wakati kamati hiyo ilipowahoji viongozi wa halmashauri hiyo ambapo, ilibaini kwa muda wa miaka mitatu mfululizo haijapeleka fedha hizo kwa wahusika hivyo kusababisha malalamiko makubwa.
Mbarouk alisema ni aibu kwa halmashauri hiyo kushindwa kufikisha fedha hizo kwa wahusika wakati serikali inazipeleka na wao kuzitumia kwa matumizi mengine.

Naye Azza Hamad (Viti Maalumu CCM), alisema hayupo tayari kuona CCM kikidhalilishwa hivyo, aliomba kamati ya nidhamu kulishughulikia suala hilo.
Alisema wamechoshwa na vitendo vya baadhi ya halamashauri kushindwa kusimamia ipasavyo fedha za maendeleo zinazotolewa na serikali na badala yake kuishia katika matumizi ya posho za wataalamu.

Kutokana na hilo, Mwenyekiti wa kamati hiyo alimuagiza mwenyekiti wa halmashauri hiyo kuhakikisha anasimamia ulipaji wa madeni hayo na suala la maendeleo ya vijana na wanawake linakuwa moja ya ajenda katika vikao vyao.