LATEST POSTS

Tuesday, December 24, 2013

MWANAMKE MWENYE NYWELE KAMA MWANAUME NIGERIA ASIMULIA STORY YAKE KWA UCHUNGU

Adai kuna mwanaume alimuahidi kumpa half million naira ili alale nae.

Na hii ndio stori yake kamili.

 
 Queen Okafor is a unique woman with unique features. She has a rare endowment from nature. Looking at her, one would think she is a man, but she is a full blooded woman.  Queen, as her name suggests, has become a celebrity of sort whenever she steps out in public as the people stare at her in amazement.  Queen’s attraction is an abundance of hairs all over her body especially in the upper region- face, hands, chests etc. Although she was born without much hair on her body, she gradually began sprouting them at the age of 21 years. Today, at 26, Queen has done many things humanly possible to stop the abnormal growth, but to no avail.

Narrating her experience, Queen said she started noticing the hair at unusual places at the age of 21.
When this reporter met Queen in a bus going to Oshodi from Mile 2, in Lagos some months ago, passengers were starring at her embarrassingly. As the lady tried to hide her face, more eyes were on her, thus arousing much interest from co-passengers.
Queen eventually opened up to this reporter, maintaining that she was not using the story to beg for money or as a form of publicity stunt, but only to draw the attention of  NGOs to fight for women with such rare disability as hers. Queen believes that she is a normal person with unwanted recognition from the society.
She told Sunday Sun:
“My name is Queen Nonyerem Okafor. I am from Anambra State. We are five children from our parents, three girls and two boys. I inherited the hairs from my mum and it runs in the family.  Once you get to 21 to 23 years  in our family, you start experiencing hair growth.  I am 26 years old now, when I was in secondary school, much hairs were not on my body. It started when I finished my secondary school. I am not granting you this interview as if I need help or money, no! I want to tell my story and what it means to be a hairy woman. All I need is for an NGO to take up my case as a woman with abnormal conditions and also to act in the movie industry.”
She revealed to Sunday Sun that the change on her skin initially made her uncomfortable, but following advice from good people, her confidence was boosted.  In her words:
“The first time it started to grow on my body, I was ashamed, but someone advised me that I shouldn’t bother, that it is a blessing not a curse. The person told me that I am unique, besides, wherever I go, I would be recognised. She advised me that I shouldn’t be ashamed, rather that I should be proud of myself. It was her that gave me strength and boosted my self esteem. Some people think that I am a man. Some think I fixed my breast to deceive people. Men especially find it difficult to believe that I am a woman. It was when we interact that most men are reassured that I am a woman. It has made me to be very popular and recognised in public. It has boosted my confidence to socialize. People want to identify with me to know the stuff I am made of. Some want to find out where this girl is coming from. People call and dash me money because of my hairy nature, but I don’t beg for money.”
Queen said she tried to stop the work of nature by applying all sorts of cosmetics and native substances, all to no avail but it turned out to cause more harm than good.

 “Before the advice came, I was asking God why all these now? I was thinking of what to rub  to clear the hair from my skin. I rubbed tortoise faeces and a lot of things people recommend for me to use, but it didn’t remove them, rather it caused more harm than good as I started growing bumps and sores while the hair was still coming out. So, I stopped rubbing those things. I suffered those lumps trying to stop the growth,” she narrated.

She revealed that her worst time comes when the weather is too hot  and during the dry season. “When there is much heat, I feel terrible, it doesn’t itch but it really inconveniences me most times. That`s why I have to wear or put on light cloths because sweat soaks my dress when I go out. Once you see me, you know that heat is dealing with me as a result of my hairy skin. I used to shave it off but if I want to shave all, it will cause me lumps all over my body. She said she had not taken the medical option seriously. “I have not gone to hospital. I don’t care anymore because it is from within my blood and it is  hereditary. I don’t need it because I can`t be using my money on something that refuses to free me. A doctor had advised that surgery can remove it, but not in Nigeria. Maybe outside the country, but I am not interested.”
Queen revealed that her hair has not changed anything in her love life, neither does it stop men from admiring her, rather it has turned many heads to look at her.
 “A man that is meant for me will come when the time comes. It is not a problem. I will get married, after all, there are other disabled people that are married despite their condition. When I was 18 or 19 years old, I was supposed to have married, but it was just that the man was a hot tempered person. He was my suitor and we ended it there. He was seeing the hair coming little by little. People are appreciating me and a lot of people are still coming for my hand in marriage.
I have been seeing many men coming to ask me for relationship, even one claimed he is from a European country that he came back to Nigeria to look for a woman to marry. But most men just want a fling, they don’t want serious relationship. I was doubting if he was real or not. I have admirers just like every other girl. Most times, I have admires more than normal girls. But most men are not sincere,  my mother would say that love is not by lip service. I have been hearing things like, I want to marry you, but after sleeping with you, the man will end up dumping you for another woman. My boyfriend likes me the way I look and I have not been dumped because I am hairy. 
Men don’t break my heart. I don’t trust men easily because I wouldn’t allow myself to have emotional breakdown. I can`t wait for my heart to be broken. In my village, an old woman has advised that she knows that I am not yet married, but I should believe that my own person is coming. She said that when my husband will come, I will find it difficult to believe that the man is my own. She told me that is how her own daughter looks. But now I have come to appreciate how I am created,” she said.
Narrating her most embarrassing moment in high density locations like market places, she disclosed that people crave to see her face.
 “I came to Lagos last year to see whether I can stay in Lagos or not. Other times I have been coming and going. But the truth is that I have been enjoying my stay in Lagos now because something good is happening. Anytime I go out, people will notice my presence and look at me. For instance, the first time I went to Ladipo Market, people besieged me, both traders and touts snapping me with their phones and video. You would be shocked how they gathered and caused chaotic situation that day, you would have written it as big news, to the extent that I went to a shopping complex and they started clapping for me, calling me Eze Nwanyi, which means Queen. They were hailing me so much. It was the most embarrassing day of my life. 
The traders and touts left what they were doing to follow me around and saying all sorts of things, if not for one man that offered to give us a lift, we wouldn’t have escaped those boys. There was a time I went to Alaba International Market with a sister and traders were peeping through the window to see my face and they were saying, ‘she is all hairs oh!’ Someone has stepped down from a bus because of me, a lady. Both of us were entering a bus at Mile 2 and immediately she glanced at me she changed her mind and immediately alighted from the bus despite that the bus conductor was urging her to enter, that was the only time someone refused to ride in the same bus with me.
Queen whose dream is to become an actress, said she was forced to resign because of sexual harassment from her employer.
“If I have the opportunity of becoming an actress, I can do that but it is to get the right person to help me. I need somebody to help me because I am perfect in everything I do. I need someone to put me through but people tell me that for some producers or directors, all they are after is to sleep with you.  I have not encountered that yet, but people have been telling me to be careful. People get easily attracted to me.
The dark complexioned Queen shocked the reporter with her revelation on how homosexuals plead to take her to bed. She also explained why she pierced her nose.
 “Why I pieced my nose was because it is fashionable, though I know I look weird already, I don’t give a hoot. It is my body,  I accept the fact that I am strange. A woman has toasted me at Elegushi Beach while I was there with my friends. On that day, she called me and gave me her complimentary card and begged me to hop into her car, but I refused. She insisted and begged to be my friend, but my mind told me that she is a lesbian and she was inviting me to Ajah. I turned her offer down because I know that most lesbians are into cultism. Some women will see me and extol my qualities, saying that they see women with hairs but that my own is the highest. In fact, one said I am the queen of hairy women. I met a guy at a supermarket and he was obsessed about me, before you knew it, he started telling me that he liked me, that I am beautiful and all that. Normal toasting, I thought he was like every other man as usual,  but after the toasting, he went straight to the point, to tell me that he would like to have sex with me through my anus, promising to give me half a million naira.
 But I rejected it immediately, God forbid! I can`t tamper with my anus.  I stopped seeing him and refused to pick his calls. I can`t do that. Another man begged me to bear him a child that will look like me, also promising to reward me handsomely. When I am praying, I plea with God to help me overcome them. Nobody can rape me because I am fearful, but men see me and get sexually aroused because I look special because of the hairy skin, but I have not been embarrassed or raped. Being hairy gives me protection as people see me and get afraid of me. Those guys who attack people see me and hail me. They will not like to do anything bad to me.
SOURCE:  MISS PETITE NIGERIA

Monday, December 23, 2013

SLAA: USHABIKI KUMFUKUZISHA ZITTO


Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe
 
Katibu  Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk.Willibrod Slaa, amesema Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, amevuliwa nyadhifa zake ndani ya chama hicho kwa misingi ya maadili na kutahadharisha kwamba ushabiki ukianza kujiingiza katika suala hilo unaweza kusababisha chama kichukue uamuzi wa kumfukuza kabisa.
Alitoa tahadhari hiyo jana wakati akizungumza na mamia ya wananchi wa mjini Nzega katika Jimbo la Nzega wilayani hapa ikiwa ni mfululizo wa ziara zake ya siku 20 katika mikoa ya Tabora, Kigoma na Singida.

Dk. Slaa ambaye hata hivyo, hakufafanua ushabiki unaofanywa katika suala  hilo, alisema Zitto alivuliwa nyadhifa za Naibu Katibu Mkuu na Naibu Mkuu wa Kambi ya upinzani Bungeni kwa misingi ya maadili kama katiba ya Chadema inavyoelekeza.

Alisema kuweka ushabiki kwa masuala ya maadili haitamsaidia Zitto bali ni kumharibia zaidi kwa kuwa chama kinaweza kuchukua hatua zaidi dhidi yake kwa kumfukuza kabisa.

Alisema msimamo wa Chadema unajulikana kutoka mwaka 2010 kwamba kabla ya kuiingia Ikulu hatua ya kwanza ni kusafisha ubovu wa maadili katika nchi hii.

“Ubovu wa maadili tusipousafisha ndani ya Chadema hatutausafisha hata tukiingia Ikulu, kama tutashindwa kusimamia maadili ndani ya Chadema basi na Ikulu tusiende sababu hatutastahili kwenda Ikulu,” alisema.

Dk. Slaa alimtaka Mwenyekiti wa Chadema mkoa wa Kigoma, Shaban Mambo, kusaidia kumshauri Zitto ili kumsaidia vinginevyo ushabiki ukiingia itakuwa ni kummaliza.

Alisema Kamati Kuu ya Chadema ilimpa siku 14 Zitto na wenzake kujieleza kutokana na tuhuma zinazowakabili ambazo zimekwisha na ameshajibu.
“Naomba nitoe tahadhari msipoangalia mtamfanya afukuzwe kweli, kama mnaomshauri hamuwezi kumshauri vizuri ikifika mahali mimi kama Katibu Mkuu ninapoona mambo yanaendelea ni lazima nitoe ufafanuzi,” alisema.

Alisema amepata taarifa kuwa baadhi ya wenyeviti wa mikoa na wilaya wameanza kupelekewa barua na fomu wazisaini ambazo wanadai zimetoka ofisi ya Katibu Mkuu wakati siyo kweli na kutaka watu wasisaini vitu wasivyovijua.

“Hizo fomu zikishasambazwa wanasema zimetoka makao makuu kwa Katibu Mkuu, msidanyanywe sijatoa fomu, sijaagiza chochote, chochote mnacholetewa kama hicho kataeni kwa sababu katiba ya chama na kanuni inaelekeza taratibu za vikao.

Tukifika mahali baadaye na haya yakiendelee mimi nisilaumiwe, nitalazimika kuyajibu,” alisema.
Kauli hiyo ya Dk. Slaa imekuja siku mbili baada ya Zitto kupokelewa kwa maandamano na wananchi wa jimbo lake juzi akitokea Bungeni mjini Dodoma.

Zitto katika maandamano hayo aliwaeleza wanachama na wakazi wa Kijiji cha Mwandiga kuwa wawe wavumilivu ili aweze kupambana hadi haki ipatikane.
“Wananchi msisikitike kwamba mtoto wenu anaonewa kwa sababu mtoto wenu ni mpambanaji.

Mimi nimevumilia sana mishale ninayorushiwa mimi kama mwanasiasa mdogo kabisa ni mingi mno, kinachoniuma mimi wananchi wangu ni kwamba mishale hii narushiwa na wenzangu wa ndani ya chama, hicho ndicho kinachoniuma, lakini kinachonitia moyo ni nyinyi wanananchi wangu,” alisema.

Alisema kila akifikiria kukata tamaa anawaza watu wa Kigoma. “Nasema watu wa Kigoma watasikitika sana acha nipambane na nitapambana, muhimu ni sharti haki kutendeka na nitahakikisha haki inatendeka.”

Aidha alisema wao walishiriki kujenga chama na wameumia kwa ajili ya chama na watakuwa wa mwisho kutoka.

Zitto alisema ni lazima waende kwa utaratibu ule ule kwa sababu wao wameweka misingi ya hicho chama na kwamba wakikimbia watakuwa wanawachia watu ambao wamekuja badaye kuja kula matunda ya kazi ambayo wameifanya.

Alisema kuvuliwa nyadhifa zake za chama siyo sahihi wala usaliti ni kwa sababu ya kutaka kugombea uenyekiti wa chama hicho Taifa na kutaka matumizi bora ya chama.

Alisema wanachama wa vyama vya siasa wanapojenga uoga kwa viongozi wao ni udikiteta, lakini viongozi wanapojenga uoga kwa wanachama hiyo ndiyo demokrasia.

Novemba 22, mwaka huu Kamati Kuu ya Chadema iliwavua uongozi Zitto, Mjumbe wa Kamati Kuu, Dk. Kitila Mkumbo na Mwenyekiti wa Mkoa wa Arusha, Samson Mwigamba kwa madai ya kukisaliti chama kwa kuanaa waraka ambao pamoja na mambo mengine ulikuwa unawakashfu viongozi wakuu wa chama hicho.
CHANZO: NIPASHE

MADIWANI BADO WAMG'ANG'ANIA MEYA TABORA

SAKATA la madiwani halmashauri ya manispaa Tabora kutaka kumg`oa mstahiki meya wa manispaa hiyo Ghulam Hussein dewji Remtullah limechukua sura mpya baada ya madiwani hao kumuandikia barua mkurugenzi kuitisha kikao cha baraza cha dharura. Madiwani hao wameandika barua hiyo mwezi disemba 10 mwaka huu yenye kichwa cha habari kisemacho ‘ombi la kuitishwa mkutano maalumu wa halmashauri kwa madhumuni ya kumuondoa madaraka mstahiki meya Ghulam Hussein Dewji Remtullah kwa kutokuwa na imani naye’. 
 
Kwa mujibu wa barua hiyo yenye orodha ya madiwani waliojiorodhesha majina na sahihi zao kutaka kumuondoa meya wao,imesema kutokana na kanuni za kudumu za halmashauri ya manispaa Tabora, kanuni namba 80 kifungu a,c na d wako sahihi kufanya hilo. “Sisi madiwani tupatao 28….tukiwa na akili zetu timamu na bila kushawishiwa na mtu yoyote tumeweka sahihi zetu hapo nyuma kutaka kumuondoa mstahiki meya kwa kushindwa kazi na kutokuwa na imani naye.”ilisema sehemu ya barua hiyo. Aidha barua hiyo ya madiwani hao inaeleza zaidi kuwa lengo la kuomba mkutano maalumu wa madiwani ni meya huyo kutumia nafasi yake vibaya,kushindwa kazi na mwenendo mbaya wa kutosimamia na kuheshimu maazimio ya mikutano. 
 
 Barua hiyo ilifafanua kuwa chini ya uongozi wa mstahiki meya huyo ameshindwa kusimamia mapato na matumizi kwa kutofikia malengo katika kujiendesha kiasi cha kuwepo ubadhirifu mkubwa na kupelekea kupata hati chafu mwaka wa fedha wa 2011/212. Aidha tuhuma nyingine ni mstahiki meya na kamati yake ya fedha,utawala na uongozi kutembelea miradi ya maendeleo na kushindwa kutoa taarifa ya ukaguzi kwenye vikao vya halmashauri toka amekabidhiwa kiti hicho. 
Meya huyo anatuhumiwa kufumbia macho ubadhirifu wa jengo la OPD kata ya Itetemia lililojengwa kwa sh milioni 100 badala ya sh milioni 40 kama alivyoelezwa mkuu wa mkoa wa Tabora Fatma Mwassa na kuwepo ubadhirifu wa ujenzi wa vyoo katika shule ya sekondari ya kata ya Ndevelwa. 
 
 Tuhuma nyingine ni safari ya Marekeani ya mstahiki meya akiongozana na mtalaam Deo Msilu mwezi april 2011 ikiwa ni ziara ya urafiki wa Millenium City ambapo safari hiyo iligharimu sh milioni 17 fedha ambazo walitakiwa kupata kibali cha halmashuri alkini hawakufanya hivyo. Aidha barua hiyo imeanisha aliyekuwa mkurugenzi wakati huo Fanuel Senge naye alisafiri kwenda nchini Ethiopia na alitumia fedha za halmashauri bila kufuata utaratibu lakini fedha hizo alirejesha na hii inamlazimu mstahiki meya naye arejeshe fedha hizo lakini amekaidi. 
 
 Katika tuhuma nyingine madiwani hao waliorodhesha jinsi meya huyo alivyojilimbikizia viwanja na kuvitaja ni Plot namba 100 area G 4070 mtrs PB chenye jina Marial Hilal, Plot namba area 158 G 6980 mtrs Ghulamhussein Remtullah, Plot namba 99 area F 3331 mtrs Dewji Ghulamhussein. Barua hiyo ilitaja viwanja vingine kuwa ni Plot namba 206 area C 2252 mtrs Gulan F Gulan,Plot namba 637 Block D 3.11 Heka 8.5 Gulam H Remtullah na hali hiyo inapelekea kuwa meya huyo amekiuka maadili ya uongozi na kutumia cheo chake kujilimbikizia mali. Aidha madiwani hao walisema tuhuma nyingine ni mstahiki meya kutumia nafasi yake kuwagwa madiwani na kutengeneza chuki kiasi cha wengine kujiuzulu nafasi zao za ujumbe wa kamati ndogo. Gazeti hili lilimtafuta mstahiki meya wa manispaa Tabora Ghulamhussein Remtullah kujibu tuhuma hizo lakini alikana na kudai ni chuki za watu, huku mkurugenzi wa manispaa huyo Alfred Luanda naye alikiri kupokea barua hiyo ya madiwani hao. 
 

SLAA AMLIPUA MAKAMU MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA URAMBO

 
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema),Dk.Willbroad Slaa akiwahutubia wananchi wa mji wa Tabora,katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Uwanja wa Shule ya Sekondari Uyui jana,akiwa ni mfululizo wa Ziara yake ya kujenga chama katika mikoa ya Kigoma,Tabora na Singida.
Katibu Mkuu wa Chadema, Dk.Willbrod Slaa, amemshukia Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Urambo, Elias Kafyenda, kutokana na tabia ya kutumia magari ya serikali kwenye shughuli zake binafsi kwa lengo la kujijenga kisiasa.
Amesema atalifikisha suala hilo kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Hawa Ghasia.

Dk. Slaa alilazimika kulizungumzia suala hilo baada ya kupewa taarifa kuwa Mwenyekiti huyo anatumia magari ya serikali kubeba wanachama wa CCM kijijini kwake kuwapeleka kwenye msiba na shughuli mbalimbali za kichama.

Taarifa ambazo zilipatikana katika mkutano wa hadhara uliofanyika kijijini hapo, Makamu Mwenyekiti huyo aliamua kuwabeba wananchi kwa magari ya halmashauri ili kuhujumu mkutano wa Chadema usiweze kufanikiwa.

“Diwani anabeba watu kwenda kwenye msiba kijiji jirani kila kunapokuwa na mkutano wa Chadema, kwanini habebi wananchi kunapotokea misiba ya walalahoi hafanyi hivyo?”alihoji.

Dk. Slaa alisema waraka wa serikali unakataza kutumika kwa magari ya serikali kwenye shughuli binafsi na kwamba CCM imekumbatia yote hayo bila kuchukua hatua kwa viongozi wanaokiuka utaratibu wa serikali.

Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Magharibi, Shaban Mambo, alisema Makamu Mwenyekiti huyo ni dhaifu ndiyo maana anakimbiza watu wasiweze kushiriki mkutano wa Chadema.

Naye Afisa wa Chadema anayeshughulikia Sera na Utafiti, Waitara Mwita, alisema diwani huyo ni mzigo ndani ya halmashauri hiyo, hivyo wananchi wasikubali kumchagua kiongozi kama huyo kwa mara nyingine.

Hata hivyo, Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Kafyenda, akizungumza na NIPASHE kwa simu alipoulizwa alisema madai hayo hayana msingi.
CHANZO: NIPASHE

Friday, December 20, 2013

MAWAZIRI WANNE WANG'OKA


Dk Emmanuel Nchimbi 
Dar es Salaam / Dodoma. Ripoti ya Kamati ya Maliasili, Ardhi na Mazingira iliyowasilishwa jana asubuhi bungeni mjini Dodoma, imewang’oa madarakani mawaziri wanne ambao wizara zao zilishindwa kusimamia vizuri utekelezaji wa Operesheni Tokomeza Ujangili.Kung’oka kwa mawaziri hao kulitangazwa bungeni jana usiku na Waziri Mkuu Mizengo Pinda aliyeeleza kuwa Rais Jakaya Kikwete ametengua uteuzi wao baada ya kuwasiliana naye kwa mashauriano akiwa nchini Marekani kwa matibabu.Mawaziri waliong’olewa kutokana na ripoti ya kamati hiyo iliyoongezewa shinikizo na michango ya wabunge wengi ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Khamisi Kagasheki, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Shamsi Vuai Nahodha na Waziri wa  Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Dk Mathayo David Mathayo.Waziri wa  kwanza kutangaza kujiuzulu alikuwa ni Kagasheki huku uamuzi wa mawaziri watatu kujiuzulu ukitangazwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.Kagasheki alitangaza kujivua wadhifa huo sa 2:09 usiku alipokuwa akichangia majumuisho ya ripoti ya kamati hiyo iliyowasilishwa na mwenyekiti wa kamati hiyo James Lembeli ambaye ni Mbunge wa Kahama (CCM).Katika maelezo yake Kagasheki alisema: “…Mimi ni mtu mzima nimesikia hisia nzito sana kwa waliyoyasema wabunge.  Rais Kikwete



aliponiteua ilikuwa ni kwa furaha yake na operesheni hii, yaliyotokea yametokea hali ya wanyama huko si nzuri;
Mimi mwenyewe nimewasikia na nachukua fursa hii kuteremka ngazi hii ya uwaziri na nitachukua taratibu za kawaida kuijulisha sehemu inayohusika(Rais).



Baada ya Kagasheki kutangaza hatua hiyo, Spika aliwaita mawaziri Dk Nchimbi na Nahodha kuchangia hoja
  hiyo, hata hivyo hawakuwepo ndipo alipoitwa Dk Mathayo na kutoa maelezo yake.

Katika maelezo yake Dk Mathayo alisema kuwa ripoti hiyo haikumtendea haki kwani kamati ya Lembeli haikumwita kumhoji na kwamba hata ripoti nzima haikueleza kuhusika na kashfa hiyo. Hata hivyo akihitimisha hoja hiyo Lembeli alisema Dk Mathayo ameshindwa kusimamia mapendekezo tisa, yakiwemo matatizo    ya wafugaji aliyopewa na Rais Jakaya Kikwete Januari 18, 2006 alipoteuliwa kushika nafasi hiyo.
Akitoa maelezo ya kutenguliwa kwa uteuzi wa mawaziri hao, Waziri Mkuu Pinda alisema: “Niliona nimtafute mkuu wa nchi (Rais Jakaya Kikwete), nilimpa picha yote ya kinachoendelea, alikubali ushauri wa Bunge; ..amekubali kuchukua ya uamuzi wa kutengua uteuzi wao(mawaziri).”

Akihitimisha mjadala huo wa ripoti ya kamati yake, Lembeli alisema: “...Katibu Mkuu na watendaji wa Wizara ya Maliasili na Utalii nao wawajibishwe kutokana na kuhusika kwao na unyama uliotokea kwenye mpango wa Operesheni Tokomeza Ujangili. Rushwa iliyopo ndani ya wizara hiyo ni kubwa inakusanywa kwa kutumia simu, hivyo Serikali izichunguze simu zao kuanzia leo.”
Michango ya wabunge
Awali hali ya hewa ndani ya kumbi wa Bunge jana ilichafuka baada ya wabunge kuchangia kwa hisia kali, wakitaka Waziri Mkuu Mizengo Pinda kujiuzulu sambamba na mawaziri wengine watatu.
Mawaziri wanaotakiwa kujiuzulu ni wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Shamsi Vuai Nahodha.
Mbunge wa Longido, Lekule Laizer (CCM), alienda mbali zaidi na kutaka Bunge livunjwe endapo Waziri Mkuu na mawaziri hao watatu watakataa kujiuzulu kwa lengo la kung’ang’ania madaraka.
Michango ya wabunge hao ilitokana na ripoti ya kamati ndogo ya uchunguzi ya Kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira chini ya Mwenyekiti wake, James Lembele iliyowasilishwa bungeni jana.
Ripoti hiyo inayohusu Operesheni Tokomeza Ujangili (OTU), ilibainisha kuwapo mauaji ya watu 13 na askari sita, utesaji wa kutisha wa watuhumiwa, ubakaji, rushwa na uporaji wa mali za wananchi.
Hata hivyo pamoja na kamati ya Lembeli kumtaka Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Dk Mathayo David apime kama bado anastahili kuongoza wizara hiyo, wabunge walimsafisha.
Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto (Chadema), alisema hakuna jinsi ya kuonyesha namna wabunge walivyokasirishwa na vitendo hivyo zaidi ya Serikali nzima kwa maana ya Pinda kujiuzulu.
“Naomba Waziri Mkuu uchukue ‘political responsibility’ (uwajibikaji wa kisiasa) na siyo kwamba kwa kufanya hivyo anahusika la hasha… Kama hachukui hatua Bunge libebe dhamana hiyo,” alisema.
Mbunge wa kuteuliwa, James Mbatia alisema ripoti hiyo ya Lembeli imetaja kuwapo baadhi ya wabunge wanaotuhumiwa kwa ujangili na kuhujumu OUT akitaka kamati iwataje ndani ya Bunge.
“Bungeni kazi yetu, sisi Wabunge ni kuisimamia Serikali kwa hiyo wale wabunge waliotajwa kwenye ripoti watajwe ili nao wawajibike ili Bunge letu liwe na nia thabiti ya kuisimamia Serikali,” alisema Mbatia.
Wabunge waliochafua zaidi hali ya hewa kutokana na michango yao ya hisia kali dhidi ya Pinda ni Mbunge wa Mwibara, Kangi Lugola (CCM), na Mbunge wa Iringa Mjini (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa.
Lugola alisema makosa ya operesheni hiyo yalianza mapema wakati operesheni ya kijeshi ilipopelekwa kwa raia na kusema; “Hainiingii akilini kwamba aliyekuwa ana command (kutoa amri) ni mwanajeshi.”

“Wakati operesheni hii ikitokea wanawake wanabakwa na watu wawili…Watu wameteswa, mwanaume mwenzetu amelazimishwa kufanya mapenzi na mti Waziri Mkuu ulikuwa wapi haya yakitokea?” alihoji.
Lugola aliongeza; ”Kwa utaratibu wa nchi yetu tumekupa kila aina ya usafiri kuanzia helikopta, ving’ora kila wakati vinalia ulikuwa wapi Waziri Mkuu wakati mambo haya machafu yanatokea?”
Alisema Vuai hawezi kupona katika suala hilo kwa kuwa wanajeshi ndiyo waliobaka, kuua na kujeruhi na ndiyo walioua mifugo kwa risasi na kwamba atapona katika Bunge hilo mbele ya haki hatapona. Vivyo hivyo alisema Dk Nchimbi hawezi kupona katika kashfa hiyo kwa vile askari polisi ndiyo walioua, kubaka, kuwapa watu vile na kuua mifugo akisema; ”Utaponea wapi Dk Nchimbi?”
Lugola alisema pamoja na ripoti ya kamati kumnukuu Kagasheki akidai alinyang’anywa mamlaka yote katika utekelezaji wa OTU, akihoji ni waziri wa namna gani aendelee kukalia kiti cha uwaziri.
“Nimeisoma ripoti hii hakuna mahali Dk Mathayo alipohusika anataka kutolewa kafara… Mifugo yake imeuliwa hahusiki na sera yeye anahusika na wafugaji waliouawa pamoja na mifugo,” alisema Lugola.
Hata hivyo Lugola alisema Dk Mathayo anahusika na uzembe kwa kuwa wafugaji imeuawa, mifugo imeuawa na kuhoji waziri huyo alikuwa wapi wakati hayo yakitokea ndani ya Tanzania.
“Naendelea kumshauri Rais kama tunaitakia mema nchi hii na kama tunataka CCM kiendelee kuaminiwa na Watanzania, Rais amfukuze Waziri Mkuu mara moja,” alisisitiza mbunge huyo.
Aliongeza kusema; “vv       Mawaziri wake hao hawawezi kukwepa hili, watu wanachukua ‘political responsibility’ kwani Maige (Ezekiel) alichukua Twiga porini?” alihoji na kuongeza kusema;
“Kama tunataka tuwe na Bunge lenye viwango, Bunge lisilokuwa na ‘double standard’ (upendeleo) na nyinyi watu wameua watu na nyinyi lazima muondoke ndiyo tutajenga heshima ya nchi hii,” alisema.
Lugola alenda mbali na kusema endapo Rais atashindwa kumfukuza Pinda katika wadhifa wake huo, yeye atakuwa wa kwanza kupeleka hoja bungeni ili wabunge wapige kura ya kumng’oa Waziri Mkuu.
Kwa upande wake, Msigwa alisema wabunge wanapopendekeza Waziri Mkuu aachie ngazi hawana chuki naye, lakini kwa madudu yaliyotokea chini ya usimamizi wake ni lazima awajibike.
“Na kama mnatuheshimu, mheshimiwa Waziri Mkuu ungekuwa unatayarisha makaratasi saa hizi unaandika barua za kujiuzulu, tukufanyie sherehe ya kukuaga na nyie wa chini yake mfuate,” alisema.
Msigwa alienda mbali zaidi na kumnyooshea kidole Vuai kwamba ana rekodi mbaya kuanzia Zanzibar na kwamba dhambi ya damu ya mauaji ya raia huko Pemba inamlilia na kumfuata hadi Bara.
“Hata sisi tunasema hamkuhusika ‘direct’ (moja kwa moja) lakini hapa tunazungumzia uhai wa watu na watu waliokufa siyo wanachama wa CCM wala wa vyama vya upinzani…Tutangulize utaifa,” alisema.
Mbunge huyo alisema siku zote cheo ni dhamana na kwamba wasingependa Chadema itakapochukua nchi iwapeleke mawaziri hao Mahakama ya Kimataifa ya Jinai, iliyopo The Heague nchini Uholanzi, kwa kuwa hawatapona.
Lekule ndiye aliyepigilia msumari wa mwisho aliposema endapo Bunge litamaliza mkutano wake huo bila kuwapo mawaziri watakaowajibika, basi Rais alivunje Bunge ili ufanyike uchaguzi mwingine.

Chanzo: Mwananchi

RAGE ASEMA, YUKO TAYARI KUJIUZULU ENDAPO WAJUMBE WA KAMATI YA UTENDAJI NAO WATAFANYA HIVYO

Mwenyekiti wa Simba, Ismail Rage.
MWENYEKITI wa Simba, Ismail Rage amesema yupo tayari kujiuzulu uenyekiti wa klabu hiyo, lakini akasisitiza hilo lifanywe na wajumbe wote wa kamati ya Utendaji.
Kwa takriban mwezi sasa hali imekuwa si shwari ndani ya Simba, baada ya baadhi ya wajumbe wa kamati ya Utendaji wakiongozwa na Kaimu makamu mwenyekiti, Joseph Itang’are ‘Kinesi’ kumsimamisha Rage kwa tuhuma mbalimbali.
Hata hivyo, Rage alikataa hatua hiyo na kusema kwamba yeye ni Mwenyekiti halali wa Simba, pamoja na hilo Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) lilimtaka Rage kuitisha mkutano wa dharura wa wanachama ili kutatua tatizo hilo, lakini Rage aligoma na kusisitiza kuwa endapo TFF itamlazimisha kufanya hivyo atajiuzulu.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Rage ambaye hakuwepo nchini kwa takribani wiki tatu zilizopita, alisema hali ilivyo kwenye kamati ya utendaji hawawezi kufanya kazi pamoja hivyo ili kuinusuru Simba ni bora wajiuzulu wote kisha uchaguzi uitishwe mapema Januari na wanaoitakia mema klabu hiyo kugombea.
Rage alisema kwanza hana sababu ya kujiuzulu wala kuitisha mkutano wa dharura kwa sababu wanachama wanaompigia kelele ni wa tawi la Mpira pesa pekee.
“Haiwezekani katika matawi 78 tawi moja tu kila siku wanaongea, wangeongea matawi 78 kidogo ningeshtuka, mimi nimechaguliwa na watu 1,820 sasa tawi la Mpira pesa sijui lina watu 204 sijui 100 ila hata sielewi lina watu wangapi,haliwezi kunipa taabu,’… “Sina mpango wa kuitisha mkutano wa dharura kama hali itaendelea hivi ya kutoelewana njia nyepesi ninayoona mwanangu (akimaanisha mwandishi aliyezungumza naye) ni kuitisha mkutano wa uchaguzi Januari kabla ya tarehe 27, ili upatikane uongozi mpya kuanzia Mwenyekiti na wajumbe wa kamati ya utendaji”.
“Tusidanganyane bwana, kamati ya utendaji hatuwezi kufanya kazi pamoja kutokana na haya yaliyotokea, ninachokifanya ni kupitia vizuri katiba inasemaje kisha nitaandika barua ya kamati ya utendaji kujiuzulu, kisha tuitishe uchaguzi Januari,” alisema Rage.
Aidha Rage alisema, pia anasubiri uamuzi wa TFF kuhusu malalamiko yake maana aliandika barua kuomba kamati ipitie maamuzi yake ya mwanzo baada ya kuona kulikuwa na dosari, na kwamba kama wakirekebisha dosari alizoziona, atakuwa tayari kufuata maagizo yao.
“Mimi binafsi siwezi kufanya kazi na kamati ambayo tayari ilishanituhumu na kunisimamisha, kwa hiyo tayari hawana imani na mimi, sasa mimi imani na wao natoa wapi, kwa hiyo tutakuwa hatuwatendei haki wanachama wa Simba. Sasa ili tuonekane wote tunafuata maadili basi ni vyema kuanzia Mwenyekiti na Wajumbe wote wa kamati ya utendaji tukajiuzulu, tukaitisha mkutano wa uchaguzi ili kuiokoa klabu yetu ili ipate mafanikio makubwa”.

CHANZO : HABARI LEO

LISHE YA MTOTO KUANZIA MIEZI 6-12


Kwa miezi sita ya kwanza katika maisha ya mtoto chakula pekee ambacho wataalamu wa afya wanashauri apewe ni maziwa ya mama tu. Kunyonyesha ndio njia ya kwanza kabisa kumpa mtoto chakula. Unapoanza kumpa mtoto vitu vingine kama maziwa ya kopo wakati ana miezi michache utoaji wako wa maziwa unaathirika maana jinsi mtoto anavyonyonya ndivyo jinsi maziwa yanavyotengenezwa ndio maana watu wengi wanavyoanza kazi na kumuacha mtoto nyumbani maziwa yao yanaanza kupungua. Faida za kunyonyesha maziwa ya mama ni pamoja na:
  1. Maziwa ya mama yana virutubisho vingi vya asili ambavyo ni muhimu sana katika ukuaji na kinga kwa mtoto. Humlinda na magonjwa mengi ya utoto pamoja na ‘allergies’ mbalimbali.
  2. Hukuwezesha kuwa na ukaribu na mtoto wako.
  3. Hukupunguzia uwezekano wa kupata kansa ya matiti.
  4. Ni bure na unaweza kumpatia maziwa wakati wowote bila usumbufu.
Wakati gani Uanze Vyakula Vingine
Mtoto wako akifikisha miezi 6 unaweza kuanza kumpatia vyakula vingine kidogo kidogo ( Kuna ambao kutokana na sababu Fulani daktari huwashauri kuanza mtoto akiwa na miezi 4 hivyo ni  vyema ukiwasiliana na daktari wako kwanza). Mtoto akianza kupewa vyakula nje ya maziwa mapema kabla ya miezi 4 ni hatari kwa afya yake maana mfumo wake wa kusaga chakula unakuwa bado haujawa tayari. Unapoanza kumpa vyakula vingine hauachi kumnyonyesha, unyonyeshaji unaendelea hadi miaka miwili na nusu.

Dalili kuwa mtoto wako yupo tayari kuanza vyakula vingine ni:
  1. Amefikisha miezi 6
  2. Anaweza kushikilia kichwa juu ( shingo imekaza)
  3. Anaweza kukaa kwa kuwekewa kitu ( mfano kiti chenye mkanda)
  4. Unapompa chakula na kijiko anafungua mdomo kutaka kupokea au anageuza uso kwa kukataa
  5. Akipokea chakula anakiweka mdomoni na kujaribu kumeza na sio kukisukuma nje na kuacha mdomo wazi.
Hakikisha mtoto wako yupo tayari kabla hujaanza kumpa chakula na usimlazimishe sana anapoanza maana anaweza kuchukia chakula, inawezekana hapendi chakula ulichompa jaribu kubadilisha uone anapenda nini. Kila mtoto ni tofauti na mwingine hivyo usimlinganishe mtoto wako na mwingine la muhimu ni kuhakikisha kuwa anauzito kulingana na umri wake na anaongezeka kwa kupanda chati.
Mnapokuwa mnakula mezani mtoto naye awe hapo ili kumpa hamu ya kula na sio kila wakati akila anakuwa peke yake. Mpe chakula akiwa na furaha na pia akiwa na njaa ili aweze kufurahia chakula chake. Kabla ya kubadilisha aina ya chakula mpe kwa siku 3-4 mfululizo ili aweze kukizoea na kama kitamletea madhara ujue hasa ni chakula gani. Usimchanganyie vyakula maana hutajua anapenda nini na kuchukia nini na pia kama kuna kitu kitamdhuru ukichanganya hautagundua kwa urahisi.

Miezi 6-9
Endelea kunyonyesha na anza kumpa vyakula vyenye madini ya chuma. Mtoto alishwe kwa ratiba inayoeleweka kila siku na katika ratiba hiyo hakikisha angalau mara moja kwa siku muda wake wa kula unakuwa sawa na muda wa familia yote ili muweze kula pamoja. Vyakula vyake viwe vimepondwapondwa kabisa ikiwezekana tumia blender na hakikisha anapata mlo kamili yani matunda, mbogamboga, mbegu, nafaka, nyama na samaki. Inashauriwa kutokuchanganya aina tofauti za nafaka kwenye unga mmoja unapomtengenezea uji, uwe na unga wa mahindi, ulezi,mchele n.k tofauti tofauti. Pika aina moja ya uji kwa wakati unaweza kufanya kwa wiki au vyovyote utakavyopenda.
 Unapompa mboga au matunda anza na tunda moja moja kwa wakati. Osha vizuri matunda yako na katakata vizuri na kuponda ponda kisha mpe kiasi kidogo kwa wakati na kikibaki usikiweke, mtengenezee kile atakachokula tu. Matunda kama papai, parachichi na embe ni mazuri kwa kuanzia. Chemsha maharage, njegere au mboga za majani na kumpa supu kidogo kidogo, usiweke chumvi nyingi kidogo sana inatosha. Usimpe juisi za madukani, hakikisha unamtengenezea juisi wewe mwenyewe na usichanganye matunda mbalimbali kwenye juisi moja, na usiweke sukari kabisa.

Miezi 9-12
Katika umri huu mtoto anakuwa tayari amezoea ladha tofauti tofauti za vyakula mbalimbali nje ya maziwa. Anauwezo wa kukaa na kushikilia kitu kwa mikono yake na kuweka mdomoni hivyo anza kumpa matunda laini mkononi aanze kujifunza kula mwenyewe. Hakikisha vipande sio vidogo sana anavyoweza kumeza ili kuepuka hatari ya kukabwa. Kwa sababu pia atakuwa ameanza kuota meno atakuwa anapenda sana kutafuna tafuna. Katika umri huu pia unaweza kuanza kumpa kiini cha yai, ute wa yai hadi afike umri wa mwaka mmoja. Endelea kumnyonyesha ila kwa sasa anakula kwanza kisha ndio ananyonya maana akinyonya sana anaweza akakataa chakula. Usimpe chakula kimoja mfululizo kwa muda mrefu maana atakinai na kuanza kukataa chakula, mpe vyakula tofauti tofauti ili aendelee kupenda chakula.

Jinsi ya Kutengeneza Chakula cha Mtoto
Ni rahisi sana kutengeneza chakula cha mtoto nyumbani kwako. Osha mikono yako vizuri kabla ya kuandaa chakula na hakikisha unatumia vyombo visafi.

Matunda na mboga mboga: osha mboga zako vizuri kwa maji safi ( ya uvugu vugu) na kisha katakata na kubandika jikoni kwa chumvi kidogo sana bila mafuta. Ikichemka isage kwenye blender au ponda ponda iwe laini kabisa kisha mpe mtoto. Matunda osha pia kwa maji ya uvugu vugu, toa ganda la nje na kata vipande vikubwa kama unataka ale kwa mikono yake mwenyewe au ponda ponda na upe kwa kijiko.

Nyama na Samaki: Chemsha vipande vya nyama na maji kidogo na iive kwa moto wa kiasi hadi ilainike kabisa kisha isage kwenye mashine (food processor) na umpe na ile supu. Samaki vile vile ila samaki hakuna haja ya kuisaga maana ikiiva inalainika sana na ni rahisi kwa mtoto kula bila taabu (Kuwa makini sana na mifupa!).

Mbegu: Hapa nazungumzia maharage, kunde, choroko, njegere n.k Pika hadi ziive kabisa na kulainika kisha pondaponda na kumpa mtoto. Pia viazi na ndizi vinafaa sana kwa watoto, unaweza ukachanganya na supu ya samaki / nyama au na maziwa.

Nafaka: Usichanganye nafaka tofauti tofauti kwa ajili ya uji wa mtoto, inashauriwa kuwa na unga tofauti kwa kila nafaka. Unapopika uji unaweza kuweka karaga zilizosagwa ili kuongeza mafuta na vitamin kwenye lishe ya mtoto.

Usalama katika Kula
  1. Hakikisha haumuachi mtoto mdogo na chakula au kinywaji bila uangalizi hata kama ni maziwa ya chupa asije akapaliwa. Usimpe mtoto chakula au maziwa akiwa amelala, analia au anacheka.
  2. Usimpe chakula ambacho kinaweza kumkaba au kumpalia kama karanga, maindi, zabibu n.k
  3. Kabla ya kumpa mtoto chakula hakikisha umekiangalia joto lake usije ukamuunguza mdomo.
  4. Usafi wa mtayarishaji, mlishaji na mlishwaji ni muhimu san asana.
Mfano wa Ratiba ya Mlo wa Mtoto
Ratiba hii ni ya mfano tu, vyakula vilivyotenganishwa na / inamaana nikimojawapo kati ya hivyo. Hakikisha vyakula havichukui nafasi ya maziwa maana ni ya muhimu kwa afya ya mtoto wako.
MUDA MIEZI 6 – 9 MIEZI 9 – 12
Alfajiri (saa 11-12) Maziwa ya mama Maziwa ya mama
Asubuhi (saa 1-2) Maziwa ya mamaUji ( Cerelac) Tunda la kupondwa pondwa Maziwa ya mamaUji ( Cerelac) Tunda la kupondwa pondwa
Kabla ya mchana (saa 4-5) Maziwa /  Kipande cha mkateMaji Maziwa / andazi / chapatti laini / Kiini cha yaiMaji
Mchana (saa 6-7) Ndizi / Viazi / Wali vya kupondwa pondwaSupu ya mboga ya majani / mbegu / samaki / nyama Tunda la kupondwa pondwa Ndizi / Viazi / Wali / UgaliMboga za majani / Nyama / Mbegu / Samaki Kipande cha Tunda
Alasiri ( Saa 9-10) Maji Maji
Jioni (saa 12-1) Uji / CerelacSupu ya mboga / mbegu / nyama / samaki Uji / CeleracMboga / Mbegu / Nyama / Samaki
Usiku ( muda wowote) Maziwa Maziwa

RAIS KIKWETE ATENGUA UTEUZI WA MAWAZIRI WANNE

Kufuatia sakata la ukiukwaji wa haki za binadamu uliofanywa na Watendaji wakati wakitekeleza zoezi la operation tokomeza majangili, Rais Jakaya Kikwete amelazimika kutengua uteuzi wa Mawaziri wanne akiwemo Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Kagesheki.

Wabunge waliongea kwa uchungu na hisia kali bungeni leo wakati wakitoa michango yao baada ya Kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira chini ya Mwenyekiti wa kamati hiyo Mhe. Lembeli kuwasilisha taarifa yao ambao imetokana na uchunguzi waliofanya katika maeneo kulikofanyika matukio hayo.

Wabunge wote bila kujali itikadi zao, waliungana kwa pamoja na kusisitiza kwamba, vitendo walivyofanyiwa Watanzania wenzetu havikuwa vya kiustaarabu, ni vya unyanyasaji wa hali ya juu na ni vya kiukwaji wa Haki za Binadamu hivyo wote waliohusika katika unyanyasaji huo wachukuliwe hatua za kisheria. Na kwa upande wa Mawaziri ambao Wizara zao zimetajwa kuhusika katika utekelezaji wa zoezi hilo nao wajiuzulu ili kurudisha imani kwa Wananchi.
Baada ya michango hiyo ya Wabunge, Mhe.Balozi Kagasheki alisimama na kutangaza kujiuzulu.
 
 Aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Balozi Khamis Sued Kagasheki.

 
 Mhe. Lisu ni mmoja kati ya Wabunge waliochangia michango ya nguvu kuhusiana na kilichojitokeza katika operation ya tokomeza ujangili
http://www.ibn-tv.com/wp-content/uploads/2012/08/KILONGO.jpg
 Mhe. Anne Kalango Malecela naye alichangia kwa nguvu zote

 
Mhe. Lema naye hakubaki nyuma.  

Sambamba na Balozi Kagesheki, wapo mawaziri wengine watatu akiwemo Waziri wa Maendeleo ya mifugo Dk. Mathayo David.

Thursday, December 19, 2013

HII NDIYO HABARI ILIYOSOMWA ZAIDI KATIKA BLOG HII KWA MWAKA 2013

Hizi picha ndio za mwanamke mrembo na mwenye mvuto kuliko wote duniani. Anaitwa Fatima Kulsum Zohar Godabari. Ni Queen wa Saudi Arabia.Na huu ni mwonekano wake akiwa hajavaa niqab.




                                                                 So beautiful






                                                                     Wouw!

                           Acha kabisa mwanawane!




Lakini swali langu la msingi ni vigezo gani hasa vinataumika ili kumpata/kumjua mwanamke mrembo kuliko wote duniani kwa sababu dunia ni pana. Waliofanya tathmini walifika na Tanzania au?


MASKINI ZITTO KABWE - CHADEMA


Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe.

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimesema hakitashughulikia rufaa iliyokatwa na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, kwa Baraza Kuu kupinga uamuzi wa Kamati Kuu (CC) wa kumvua nyadhifa zake katika chama, hadi hapo itakapopitia utetezi wake na kuamua hatima ya uanachama wake katika chama hicho.
Pia kimethibitisha kupokea utetezi dhidi ya mashitaka 11 yanayohusisha usaliti dhidi ya chama na kuwachafua viongozi wakuu kupitia waraka wa mabadiliko.
Mashtaka hayo yanamkabili Zitto, pamoja na aliyekuwa Mjumbe wa CC, Dk. Kitila Mkumbo na aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Arusha, Samson Mwigamba.
Kaimu Katibu Mkuu wa Chadema, Victor Kimesera, alisema hayo alipozungumza na NIPASHE, ofisini kwake, jijini Dar es Salaam jana.
Kimesera, ambaye ni Katibu Mtendaji Ofisi ya Katibu Mkuu wa Chadema, alisema rufaa hiyo ni kitu kidogo, hivyo haiwezi kuanza kushughulikiwa na chama katika sakata la Zitto na watuhumiwa wenzake.
“Kuna (kitu) kikubwa cha mbele yake (rufaa),” alisema Kimesera akijibu swali la NIPASHE lililotaka kujua nini kinaendelea kwenye chama baada ya Zitto kukata rufaa.
 Kimesera alisema kitu kikubwa kuliko rufaa, ambacho kitaanza kushughulikiwa na chama ni maelezo ya utetezi wa Zitto na watuhumiwa wenzake.

Alisema hiyo ni kwa sababu tayari kuna hoja ya CC, ambayo inataka ijiridhishe kama Zitto na wenzake waendelee kuwa uanachama au la.

 Kwa mujibu wa Kimesera, baada ya Zitto na wenzake kuwasilisha utetezi wao, CC itaitishwa na kuyapitia na kisha itatoa maamuzi juu ya uanachama wao.
“Sasa huwezi kuongea juu ya rufaa wakati hujajua uanachama wao kwanza,” alisema Kimesera.

 Hivyo, alisema rufaa ya Zitto itaendelea kuhifadhiwa kwenye jalada hadi hapo hatua ya kwanza ya kupitia maelezo yao ya utetezi na kuyatolea maamuzi itakapochukuliwa. “Lazima twende kwa hatua. Kwa hiyo, hiyo (rufaa) imekaa,” alisema Kimesera.

 Mwanasheria wa Zitto, Albert Msando, alitaja sababu mbili za mteja wake kukata rufaa kuwa ni kukiukwa kwa taratibu za kuchukua hatua za nidhamu na sababu zilizotolewa kutokuwa sahihi.

Msando alitaja kifungu cha 6.5.6 cha Kanuni ya Uendeshaji ya chama hicho, akisema utaratibu uliotakiwa kufuatwa kabla ya kumchukulia hatua za kinidhamu kiongozi kwa mujibu wa Katiba na Kanuni ni kupewa kwanza mashtaka kwa maandishi ili apate nafasi ya kujibu.

 Alisema kiongozi yeyote hatachukuliwa hatua za kinidhamu bila kwanza kupewa mashtaka yake kwa maandishi na mamlaka husika na kupewa nafasi ya kujibu mashtaka kwa maandishi.

Alitaja  ibara ya 5.4.3 na 5.4.4 ya Katiba kwamba mwanachama yeyote hatachukuliwa hatua za kinidhamu ama kuonywa ama kuachishwa ama kufukuzwa uanachama bila kujulishwa makosa yake kwa maandishi na kutakiwa kutoa majibu katika muda usiopungua wiki mbili.”

 Alitaja vipengele vingine ni kupewa nafasi ya kujitetea mbele ya kikao kinachohusika na atajulishwa kwa maandishi uamuzi wa kikao ndani ya wiki mbili baada ya kusikilizwa.

 Katika hatua nyingine, Kimesera alisema Chadema imepeleka majibu baada ya Mwigamba kupeleka barua yenye malalamiko kwa Msajili wa Vyama vya Siasa dhidi ya uongozi wa chama hicho.

Katika malalamiko yake, Mwigamba anadai kuwa katiba ya Chadema ilivurugwa na viongozi wa chama kwa kuondoa kinyume cha taratibu maelezo ya kifungu cha katiba ya chama yaliyokuwa yakiainisha ukomo wa vipindi viwili vya uongozi.

 Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi, alithibitisha kupokea barua hiyo ya Mwigamba na kusema ofisi yake inaifanyia kazi.

 Kimesera jana aliliambia NIPASHE kuwa walipeleka majibu dhidi ya malalamiko ya Mwigamba baada ya kuagizwa na msajili kufanya hivyo kabla ya Desemba 19, mwaka huu.

 Katika barua yake, Mwigamba amemuomba msajili kutoa mwongozo kuhusu anachodai kuwa ni mgogoro wa kikatiba uliopo ndani ya Chadema kufuatia kipengele cha katiba kinachogusia ukomo wa uongozi kubadilishwa kinyume cha utaratibu.

 Novemba 22, mwaka huu, CC iliwavua madaraka viongozi hao na kuwataka wajieleze kwa maandishi ndani ya siku 14 baada ya kudaiwa kuhujumu chama kwa kuandika waraka wa siri unaodaiwa pamoja na mambo mengine, kuwadhalilisha viongozi wakuu wa Chadema.
 
CHANZO: NIPASHE

MTOTO WA MBARAKA MWISHEHE AJERUHI WAWILI DAR




MASIKU Mbaraka Mwishehe ametiwa mbaroni na Jeshi la Polisi Kinondoni, Dar es Salaam kwa madai ya kuwashambulia kwa kisu watu wawili wa familia moja.


Tukio hili lilitokea hivi karibuni Mwananyamala Kisiwani, Dar ambapo kwa mujibu wa taarifa ya kipolisi, mtuhumiwa huyo alikutwa ndani ya nyumba ya Nelson Ainea Shoo, saa kumi na moja alfajiri.
Akizungumza na Amani, mke wa Nelson aliyejitambulisha kwa jina la Neema Hamis Zame (32), alikuwa na haya ya kusema:
“Siku ya tukio, ilikuwa alfajiri kabla hatujaamka, ghafla nilimsikia shemeji yangu aitwaye Goodluck (Ainea Shoo) akipiga kelele na kusema: ‘Kaka kuna mwizi.’ Mume wangu aliamka akatoka kuelekea sebuleni na mimi nilikuwa nyuma yake.


“Kufika, tulimkuta shemeji amelala sakafuni huku utumbo ukiwa nje na damu nyingi zikimtoka, alikuwa akikoroma, kumbe alichomwa kisu kwenye paja, mara mbili tumboni na begani.
“Nilikimbilia chumbani kuchukua khanga na kumfunga ili kuzuia damu isitoke kwa wingi, pia utumbo usiendelee kumwagika huku mume wangu akimdhibiti yule mtu.
“Cha ajabu, muda mfupi mume wangu naye akawa chini anatokwa damu, kumbe hata yeye alikuwa amechomwa kisu mara tatu tumboni na utumbo ukatoka nje.
“Hali ndani ilikuwa mbaya, sakafu ilitapakaa damu. Nikamwita shemeji yangu mwingine aitwaye Erick (Ainea Shoo), yeye akapambana na yule mtu wakati mimi nawahudumia wale majeruhi.



“Nilipata akili za haraka, nilikwenda kumuita mlinzi akaingia na kushirikiana na shemeji wakamdhibiti. Huwezi kuamini, eti yule mtu akaomba asamehewe kwa vile hakujua kama alikuwa ameingia katika nyumba yetu.
“Hakuna aliyemsikiliza kwani alikuwa amefanya kosa kubwa, akaingizwa kwenye gari hadi polisi kuchukua PF3 na likafunguliwa jalada (OB/RB/20201/2013 Kujeruhi) kisha majeruhi tukawapeleka Hospitali ya Muhimbili.
“Kilichotokea hospitali,  shemeji alitolewa bandama kwa vile iliharibika kutokana na majeraha ya kisu,” alisema Neema.
Naye baba mzazi wa majeruhi hao, mzee Ainea Shoo ambaye alitoka Machame Moshi, Kilimanjaro baada ya kupata taarifa hizo, alisema mtuhumiwa huyo alikuwa na dhamira ya kuwatoa roho watoto wake hao, akaliomba jeshi la polisi kushughulikia kesi hiyo kwa uwazi na kuhakikisha haki inatendeka.



Mlinzi wa nyumba hiyo, Boli Mtumwa alipohojiwa na gazeti hili alikiri kutokea kwa tukio hilo na kusema yeye na mdogo wa Nelson ndiyo waliomdhibiti mtuhumiwa na kumpeleka polisi.
Dada wa mtuhumiwa aliyejitambulisha kwa jina la Taji Mbaraka alikiri kukamatwa kwa kaka yake huyo lakini hakuwa tayari kuzungumza zaidi kwa sababu suala hilo lipo mkononi mwa dola.
Kaimu Kamanda wa Mkoa wa Polisi Kinondoni, ACP Yusuf Mrefu alikiri kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa mtuhumiwa anaendelea kushikiliwa huku upelelezi ukiendelea.
Chanzo: GPL

WAKULIMA SABINI WA CHAMA CHA MSINGI LUGANJO WAFUTWA UANACHAMA


Wakulima Sabini na Saba wa chama cha Msingi cha Ushirika cha Luganjo,Kata ya Usinge, wilaya ya Kaliua, wamefutwa uanachama kwa madai ya kulaza madeni hatua ambayo imelalamikiwa kuwanyima haki ya kupata pembejeo kwa msimu huu wa kilimo.
Wakizungumza kwenye Mkutano wa hadhara kijijini Usinge, wakulima hao wamesema hatua hiyo iliyochukuliwa na Afisa Ushirika wa wilaya ya Kaliua, Happiness Mwangomole ni ya uonevu kwa sababu katika msimu uliopita wa kilimo wamelipa madeni yao kwa kati ya asilimia 58 na asilimia 90.
Wamesema wakulima 77 waliofutwa katika chama cha msingi ni wale ambao wamekuwa wakiilalamikia Serikali ya kijiji kwa kutosimamia kikamilifu Maendeleo ya wananchi na kufichua ubadhirifu unaofanywa na viongozi wa serikali ya kijiji hicho.
Mwenyekiti wa CCM wa kijiji hicho, Clement Bigambana amemwomba Mrajisi wa vyama vya ushirika Dodoma kuingilia kati ili kuwasaidia wakulima hao waliofutwa uanachama ili wakopeshwe pembejeo za kilimo kwa lengo la kuwakwamua kujikwamua kiuchumi, kwani uchumi wao unategemea kilimo cha tumbaku.
Katika mkutano huo, wananchi wa Usinge pia wamelalamikia uongozi wa serikali ya kijiji kushindwa kutoa taarifa ya mapato na matumizi ya fedha za miradi kutoka Serikali kuu kwa muda wa miaka minne sasa na kushindwa kuwachukulia hatua wananchi wana0shawishi wengine kugoma kuchangia asilimia 20 ya miradi ya maendeleo.

Wednesday, December 18, 2013

Kigoma yazalisha tani 5,000 za tumbaku

MKOA wa Kigoma unazalisha tumbaku zaidi ya tani 5,000 kwa mwaka.
Naibu waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Adam Malima alitoa kauli hiyo bungeni mjini hapa jana akijibu swali la Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila (NCCR-Mageuzi), ambaye alitaka kujua ni kwa nini mpaka sasa mkoa huo haujapewa hadhi ya kuwa mkoa wa Kitumbaku ili kusogeza huduma kwa wakulima ambao kwa sasa wanategemea huduma kutoka Urambo.
Alifafanua kuwa mkoa wa Kigoma ni miongoni mwa mikoa inayozalisha tumbaku nchini ambapo zaidi ya tani 5,000 huzalishwa kwa mwaka.
Malima alisema mkoa huo umepitishwa kulima tumbaku kwa mujibu wa sheria ya tumbaku namba 24 ya mwaka 2001 na kanuni zake za mwaka 2005.
Aidha, alisema pamoja na kiasi hicho cha uzalishaji mkoa wa Kigoma haujapewa hadhi ya kuwa mkoa wa Kitumbaku kutokana na changamoto ya upatikanaji wa fedha ili Bodi ya Tumbaku iweze kufungua ofisi na kusogeza huduma karibu kwa wakulima wa zao hilo kama ilivyo kwa mikoa mingine ya kitumbaku.
Alisema kwa kutambua mchango wa wakulima wa tumbaku wa mkoa wa Kigoma, serikali kupitia Bodi ya Tumbaku katika mwaka wa fedha 2013/14 inatarajia kufungua ofisi zake mkoani Kigoma ili kusogeza huduma kwa wakulima wa zao hilo.
Chanzo:Tanzania Daima

MARUFUKU HALMASHAURI KUFANYA VIKAO VYA HALMASHAURI BILA WABUNGE

HALMASHAURI zote za wilaya nchini zimepigwa marufuku kuandaa vikao vya halmashauri bila kutoa taarifa kwa wabunge kwa sababu nao wana haki ya kuhudhuria vikao hivyo Kikatiba.
Hayo yalielezwa Bungeni  mjini hapa jana na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Aggrey Mwanri, alipokuwa akijibu swali la nyongeza la mbunge wa Kasulu Mjini, Moses Machali (NCCR-Mageuzi).
Mbunge huyo alitaka kujua, Serikali inazichukulia hatua gani baadhi ya halmashauri nchini zikiwemo za Kasulu na Kibondo, ambazo huandaa vikao vya halmashauri bila kuwaita wabunge na  hasa wakati vikao vya Bunge vikiendelea.
Mbunge huyo pia, alihoji ni kwa nini makatibu wa wabunge hata wakiingia kwenye vikao hivyo hawalipwi posho kwa madai kuwa si wajumbe wa vikao wakati maofisa tarafa na watendaji wanalipwa posho hizo pindi wanapoingia kwenye vikao hivyo.
Akijibu swali hilo, Mwanri alisema tayari Serikali imeandaa taarifa itakayopelekwa kwa halmashauri zote nchini kuhakikisha kuwa zinaandaa vikao kulingana na ratiba za Bunge ili wabunge ambao ni wajumbe wa vikao hivyo nao wapate fursa ya kuhudhiria.
Alisema kikatiba Wabunge  nao ni madiwani wana haki zote za kuhudhuria vikao vya halmashauri, na kupiga marufuku halmashauri zote nchini kuandaa vikao vya halmashauri bila kumpa taarifa mbunge.
“Huyu mbunge ana mchango mkubwa kwenye vikao hivi, anahudhuria vikao vikubwa kama Bunge, hivyo ana uzoefu na uelewa mkubwa,” alisisitiza Mwanri.
Aidha Kuhusu posho kwa maofisa tarafa, Naibu Waziri huo alikiri kuwa huwa wanalipwa posho wakiingia kwenye vikao hivyo, kwa sababu wao ni wasaidizi wakubwa wa Mkuu wa Wilaya na wanatambulika kisheria wakati makatibu wa Bunge pamoja na kuwa na sifa ya usaidizi kwa mbunge bado hawajatambulika kisheria kuweza kulipwa posho katika vikao hivyo.
Alisema upo uwezekano wa suala hilo kushughulikiwa  kwa wabunge kuwasilisha maoni na mapendekezo ya kuibadilisha Sheria iliyopo ya halmashauri ambayo itaweza kuwatambua makatibu wa Bunge kama wasaidizi wa wabunge na walipwe posho kwenye vikao hivyo.

RPC TABORA AMKINGIA KIFUA MTUHUMIWA

Kamanda wa Polisi  mkoani Tabora, Peter Ouma
 Kamanda wa polisi Mkoa wa Tabora

HATMA ya Mkuu wa Kituo cha Polisi Igunga mkoani Tabora, SP Edson Mfuru anayedaiwa kumuachia mtuhumiwa Magata Singu anayetuhumiwa kumpa mimba mwanafunzi wa darasa la sita mwenye umri wa 14 katika Shule ya Msingi Hani Hani, iliyopo Igunga sasa ipo mikononi mwa kikosi cha kupambana na rushwa (TAKUKURU).
Wakati TAKUKURU wakiingilia kati suala hilo, taarifa zaidi zinasema kuwa Kamanda wa Polisi mkoani Tabora, Peter Ouma anafanya jitihada za kumnusuru SP Mfuru asikabiliane na mkono wa sheria.
Hatua ya RPC Ouma kuhusishwa kumuokoa SP Mfuru, inatokana na madai ya kushindwa kuwachukulia hatua askari wanaodaiwa kuchana karatasi iliyoandikwa maelezo ya binti aliyelalamika (RB) pamoja na ile ya mtuhumiwa kukamatwa kwa mara ya kwanza.
Uamuzi wa TAKUKURU umekuja siku chache baada ya Kamanda Ouma kukutana na OCD wa Igunga, Abed Maige pamoja na OCS Mfuru katika kikao cha ndani ambapo maofisa hao wa polisi walimueleza RPC namna siri za polisi zinavyovujishwa, na kumuomba awasaidie kukabiliana na hali hiyo.
Katika kikao hicho cha ndani, inaelezwa kuwa RPC Ouma aliwaeleza wazi kuwa kukithiri kwa rushwa na kudhulumiana ndiyo chanzo cha baadhi ya mambo ya polisi kuvuja hadharani.
Hata hivyo, katika kikao hicho inaelezwa kuwa lilitolewa agizo la kuwahamisha baadhi ya askari waliotuhumiwa kuwa nyuma ya siri za kuachiwa mtuhumiwa Singu.
Jambo jingine lililosababisha TAKUKURU waingilie kati ni pamoja na mtu aliyemwekea dhamana Singu kuendelea kuwa nje huku mtuhumiwa aliyewekewa dhamana akiwa hajulikani alipo.
“Bado hali ni mbaya na sasa TAKUKURU wameshaingilia kati kwa kuanza kumhoji mlalamikaji na pia kutaka kujua sababu za mtuhumiwa kutofikishwa mahakamani,” kilisema chanzo chetu ndani ya Jeshi la Polisi Igunga.
Kwa mujibu wa habari hizo, miongoni mwa watu watakaotoa maelezo mbele ya TAKUKURU ni pamoja na askari aliyemkamata mtuhumiwa na yule aliyeshika faili la kesi kabla ya mtuhumiwa kuachiwa.
Kamanda wa TAKUKURU Wilaya ya Igunga, John Ngunangwa alipoulizwa juu ya kikosi chake kuingilia kati suala hilo, alikiri kulifuatilia huku akikataa kutoa maelezo zaidi kwa ajili ya kukamilisha taratibu za kuwakamata wahusika.
RPC Ouma alipoulizwa hatua zilizochukuliwa na Jeshi la Polisi kwa watuhumiwa, alisema bado wako kwenye uchunguzi.
Alipotakiwa kueleza kama kunahitajika uchunguzi zaidi ya kuanzia katika kitabu cha kumbukumbu ya matukio ya polisi na kufuatilia namba aliyopewa mlalamikaji katika tuhuma hizo, RPC Ouma alisema yupo katika kikao na kukata simu.
Hivi karibuni, gazeti hili liliandika juu ya mtuhumiwa Magata Singu kuachiwa kwa dhamana ya sh mil. 3.4 kutokana na tuhuma za kumpa mimba mwanafunzi wa darasa la sita mwenye umri wa miaka 14.
Ilielezwa kuwa Novemba 9, wazazi wa mtoto huyo walifika katika Kituo cha Polisi Igunga na kufungua mashitaka na kupewa namba ya jalada, RB IG/1430/2013 na kisha mtuhumiwa kukamatwa Novemba 10 na kuachiwa Novemba 11.
Chanzo: Tanzania