LATEST POSTS

Monday, November 23, 2015

Rais Magufuli afuta sherehe za uhuru



sefue (2)Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue
KATIBU Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue ametoa taarifa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk John Pombe Magufuli amefuta sherehe za uhuru mwaka huu na badala yake, Desemba 9 itakuwa siku ya usafi nchi nzima ili kuondokana na tatizo la kipindupindu linaoikabili nchi.
Balozi Ombeni ameongeza kuwa, wakuu wa mikoa na wilaya zote wajiandae kuandaa vifaa vya vya usafi kwa ajili ya shughuli hiyo.
“Rais Magufuli ataangalia bajeti iliyokuwa imeandaliwa kwa ajili ya sherehe hizo, kisha ataielekeza kwenye sekta au wizara  atakayoona inauhitaji ili zikasaidie kule.
“Haipendezi kusherehekea miaka 54 ya uhuru huku kipindupindu kikituua, hivyo usafi ni muhimu kwa ajili ya afya zetu,” alisema Balozi Ombeni.
Hayo yamejiri wakati Balozi Ombeni alipofanya ziara kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili kukagua mashine za MRI na zile za CT-Scan na vitanda vilivyonunuliwa kutokana na agizo la Rais Magufuli kuamuru pesa zilizokuwa zimeandaliwa kwa ajili ya bajeti ya sherehe za ufunguzi wa Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano, mjini Dodoma Alhamisi iliyopita zielekezwe Muhimbili kununua vitanda vya wagonjwa.

0 comments: