LATEST POSTS

Thursday, December 5, 2013

ELIMU YA MATUMIZI YA NISHATI MBADALA KUNUSURU MAZINGIRA

 
WANANCHI
 
 waishio maeneo ya Vijijini endapo watapata elimu kuhusu matumizi ya
 
 Nishati mbadala,watakuwa katika nafasi nzuri ya kutunza mazingira 
 
yanayoharibiwa kwa kasi kutokana na matumizi ya kuni katika kukaushia 
 
tumbaku na matumizi ya Nyumbani. 
 
Akifungua mafunzo kwa walimu wa Umeme Vijijini wa Vyuo vya Maendeleo ya 
 
Jamii,Mkuu wa Wilaya ya Uyui,Bi Lucy Mayenga katika Hotuba yake 
 
 
iliyosomwa na Katibu Tawala,Bw.Bibangamba John,ameeleza ni lazima elimu 
 
ya matumizi sahihi ya Nishati mbadala itolewe ili wananchi wasizidi 
 
mazingira. 
 
Ameeleza wananchi wanatumia sana kuni na kuharibu mazingira lakini 
 
matumizi ya Nishati mbadala yatawasaidia sana kuokoa na kutunza 
 
mazingira ambayo ni muhimu kwa ustawi wa maisha yao. 
 
Mayenga amesisitiza kwa wshiriki hao kuhakikisha kweli wanaipeleka elimu 
 
 hiyo kwa wananchi wengi waishio vijijini vinginevyo itakuwa ni kazi 
 
bure. 
 
Kwa upande wake Afisa Kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia na 
 
watoto,Pius ligo,amesema Wakala wa Nishati Vijijini,REA, wanataka 
 
wananchi wasitumie Nishati inayoharibu mazingira. 
 
Amesema mafunzo hayo yanayotolewa kwa washiriki kutoka Mikoa Tisa Nchini 
 
 yatatumika kueneza elimu ya matumizi ya Nishati mbadala kwa wananchi wa 
 
Vijijini kupitia washiriki hao na hivyo kuleta ustawi wa maisha ya 
 
wengi 
 
Mafunzo hayo yanayochukua Wiki mbili yanayoendeshwa na wakala wa Nishati 
 
Vijijini,REA kwa kushirikiana na Wizara ya maendeleo ya 
 
Jamii,yatawapeleka washiriki kufunga Nishati katika zahanati ya Miyenze 
 
ambayo itakuwa ni sehemu ya mafunzo yao.
 
CHANZO: TABORA YETU

0 comments: