LATEST POSTS

Wednesday, February 17, 2016

Kitunguu Swaumu, Mafuta ya Mzaituni kwa kutibu sikio


kitunguu swaumu 
Wiki hii utaelekezwa namna unavyoweza kutibu sikio kwa kutengeneza dawa nyumbani kwako ambayo ni mafuta ya mzaituni na kitunguu swaumu.
Vitu vinavyohitajika
Punje moja ya kitunguu swaumu iliyosagwa na vijiko 2 vya mafuta ya mzaituni
Oleacanthal-the-key-benfit-of-olive-oil 
Jinsi ya kutengeneza dawa
Njia ya kwanza ni ya kupasha moto mafuta ya mzaituni kisha kuchanganya na kitunguu kilichosagwa. Mchanganyiko huu unaachwa upoe, kisha unadondoshwa kwenye sikio. Hii hutibu na kutuliza maumivu haraka kutokana na ujoto wa dawa hiyo.
Njia ya pili ni kuchukua kitunguu swaumu, kukisaga kisha kuchanganya na mafuta ya mzaituni, halafu mchanganyiko unaachwa kwa saa mbili hadi tatu, kabla ya kutumika. Baada ya kutengenezwa kwa dawa hii, mtumiaji atatumia kwa kudondoshea matone mawili sikioni wakati wa asubuhi na atafanya hivyo tena jioni. Ni dawa isiyo na madhara kwa mtumiaji.
Hatua hii ya pili si rahisi sana kukupa ahueni kama hiyo ya kwanza.

Source: Global publishers

0 comments: