LATEST POSTS

Monday, October 13, 2014

LILE TUKIO LA MELI KUZAMA KOREA KUSINI LATENGENEZEWA FILAMU

WAANDAAJI wa tamasha kubwa la filamu  Korea Ya kusini BUSAN wametetea uamuzi wao wa kuonesha  filamu iliyoleta utata nchini humo ya  Driving Bell, 'The Truth Shall Not Sink With Sewol'
Filamu hiyo inayoelezea maafa ya majini yaliyo ikumba nchini hiyo  imeonyeshwa kwa mara ya kwanza siku ya mwisho ya tamasha hilo kwa kuhudhuriwa na idadi kubwa ya watu kuliko filamu zote.
Tamasha hilo ambalo lime hitimishwa hapo jana ilionesha kwa mara ya kwanza filamu hiyo fupi inayolezea kwa ujumla jinsi uokoaji ulivyofanyika na kushuhudia Wananchi wa korea kusini wakihangamia katika ajali hiyo ya majini iliyotokea nchini humo mwezi April mwaka huku ikidaiwa kupoteza maisha ya watu zaidi 300.
Waandaji wanasema kuwa watu wanahitaji kutoa maoni yao na sauti zao zisikike, na kila filamu inayooneshwa katika tamasha hilo ina umuhimu kwa wananchini na wapo tayari kuwajibika endapo lolote litatokea.
Muandaaji
Hapo awali ilitaarifiwa kuwa waaandaji hao waliambiwa waiondoe filamu hiyo kwenye orodha ya filamu zitakazooneshwa ikiwa ni shinikizo kutoka kwa baadhi ya wanasiasa akiwemo meya wa jimbo la Busan.
Uamuzi wa kuonesha filamu hiyo fupi umeiletea sifa waandaji wa filamu hiyo baada kusifiwa na muandaaji wa filamu fupi za Marekani Joshua Oppenheimer.

0 comments: