LATEST POSTS

Monday, July 6, 2015

Mkojo wa paka sasa wageuka ‘dili

 
 
Paka ni mnyama rafiki anayependwa na binadamu. Ni mnyama pekee  anayeweza kuishi na binadamu ndani ya nyumba moja tofauti na wanyama wengine.
Katika maisha ya kawaida ya mwanadamu hasa jamii Afrika, paka hutumika pia kama mlinzi kuzuia au kudhibiti panya ndani ya nyumba kwa kuwakamata na kuwa mlo wake.
Lakini Waswahili husema; “tembea uone mambo.”
Usemi huo umetimia kwangu baada ya kufika mkoani Morogoro, hivi karibuni na kutembelea Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA).
Katika chuo hicho, wasomi wazalendo ambao ni watafiti wa masuala ya kilimo na ekolojia ya panya, wamebaini kwamba mkojo wa paka unaweza kutumika kama njia ya  kufukuza panya kwenye mashamba na makazi ya watu.
Tofauti na wengi walivyozoea kwamba paka hutumika  kufukuza panya nyumbani, lakini sasa kwa ugunduzi wa wataalamu hao  mkojo wa mnyama huyo rafiki wa binadamu
pia unaweza kufanya kazi hiyo. Mkuu wa mradi huo katika Kitengo cha Kudhibiti Viumbe Waharibifu Shambani kutoka SUA, Profesa Loth Mulungu anasema kwamba walianza mradi huo mwaka 2012, lengo likiwa kudhibiti panya.
“Tulitafiti ili kuwezesha mkojo wa paka kutumika kama kiuatilifu cha kufukuza panya nyumbani na kwenye mashamba,” anasema Profesa Malungu.
Anasema kuwa mradi huo unadhaminiwa na Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), na ulianzishwa kama moja ya njia mbadala za kukabiliana na panya waharibifu.
“Panya ni kiumbe mharibifu shambani, hata nyumbani. Ili kumwangamiza, zimekuwapo njia mbalimbali za kuwadhibiti ikiwamo utumiaji wa sumu ambayo si rafiki wa mazingira pamoja na afya za binadamu.
Pia inatokea, nao panya wakigundua mwezao mmoja amekufa kwa kula chakula chenye sumu, wanaobaki hawali tena chakula hicho,”anasema na kuongeza:
“Lakini kwa huu mkojo wa paka, wakinusa harufu watakimbia wakidhani paka yupo kwenye eneo husika.”
Mkojo unavyodhibiti panya
Akizungumzia mkojo huo unavyodhibiti panya, Profesa Mulungu anasema utafiti umeonyesha kuwa mkojo wa paka jike una harufu kali ikilinganishwa na ile ya paka dume na ndiyo panya akiinusa anakimbia na harudi eneo husika.
Profesa Mulungu anaeleza kuwa: “Utafiti bado unaendelea ili kupata viini vilivyoko kwenye mkojo huo kabla ya kutengenezwa kwenye maabara. Utafiti wetu umebaini kuwa mkojo huo unafanya kazi kwa asilimia 100.”
Anabainisha kuwa ingawa kazi ya utafiti huo haijakamilika, umefanikisha kubaini aina mbili za viini kwenye mkojo wa paka, ambavyo humfanya panya agundue kuwa harufu husika ni ya paka.
“Utafiti ukikamilika na kiwatilifu kikatengenezwa, tutakuwa na jibu zuri zaidi na kufanikisha tafiti yetu. Kiwatilifu hi
Licha ya mradi huo, SUA pia inafanya mradi mwingine wa utafiti wa panya kwa kutumia njia za ekolojia, ambapo makamu mkuu wa chuo kikuu hicho Profesa Gerald Monela anasema:
“SUA inaahidi kutumia uwezo, ubunifu na utalaamu wa watafiti wake katika kusaidia kudhibiti tatizo la panya waharibifu wa mazao ambao wamekuwa wakisababisha hasara kubwa kwa wakulima nchini kila mwaka.”
Anasisitiza: “ Tanzania pekee hupoteza zaidi ya tani 400,000 za mahindi kila mwaka kutokana na uharibifu unasababishwa na panya.”
Anabainisha kuwa chakula hicho kinachopotea kingeweza kutosha kulisha zaidi ya Watanzania milioni mbili kwa mwaka mzima, hivyo ni kiasi kikubwa cha upotevu.
Anaongeza kuwa mbali tatizo la upotevu wa chakula, pia panya husababisha magonjwa mbalimbali ikiwemo ugonjwa wa tauni.
Profesa Monela anasema kuwa SUA ina wataalamu wenye weledi wa kudhibiti tatizo hilo na tayari mafanikio makubwa yameonekana nchi nzima kutokana na usaidizi wa chuo kikuu hicho.
Mradi huo unazijumuisha taasisi mbalimbali za hapa nchini kama zikiwamo Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine, Chuo Kikuu cha Da es Salaam (UDSM), Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu cha Chang’ombe (DUCE), Chuo Kikuu cha Muhimbili(MUCHS katika taasisi ya tiba asilia na Chuo Kikuu cha Dodoma.
Mwaka 2012 katika maonyesho ya Taasisi za Elimu ya Juu yaliyofanyika jijini Dar es Salaam, mtafiti wa kituo cha utunzaji wadudu kilichoko chini ya SUA, Profesa Christophar Sabuni alisema kuwa kituo hicho kinafanya utafiti utakaosaidia wananchi kupata njia mbadala na salama kwa binadamu ya kufukuza panya sehemu mbalimbali, badala ya kutumia sumu kama inavyofanyika sasa.
“…Hasa tukilenga kwenye mazao na makazi ya watu, utafiti huu unalenga kumsaidia mwananchi kufukuza panya na kuondoa uharibifu. Wanaopata adha kubwa ya wanyama hawa ni wananchi, hivyo utafiti huu utawasaidia sana,” alisema Profesa Sabuni.
Alifafanua kwamba mchakato wa utafiti huo ulianza kwa kuangalia ni haja ndogo ya paka wa jinsia ipi unaoweza kupata dawa ya kufukuza panya na kugundua kuwa paka wa jike ni bora zaidi.
“Unapofanya utafiti, huna budi kuangalia njia itakayosaidia kutimiza lengo haraka, tukaamua kuangalia jinsia dume na jike na kugundua kuwa harufu ya mkojo wa paka jike itatufaa zaidi,” alisema.
Alisema kupitia utafiti wao, wanalenga kuichakata haja ndogo hiyo kutoka kimiminika hadi kuwa katika hali ya ungaunga ili kurahisisha utumiaji wake kama dawa.

Alibainisha kuwa utafiti unatarajiwa kuchukua wastani wa miaka mitano ikiwa ni mwendelezo wa tafiti mbalimbali zilizowahi kufanywa na kituo hicho.
Profesa Sabuni alieleza kwamba, awali utafiti huo ulihusisha utafiti wa mafunzo ya panya kwa ajili ya kugundua mabomu yaliyotegwa ardhini na kugundua vimelea vya kifua kikuu katika makohozi.
Naibu makamu mkuu wa chuo hicho, Profesa Yunika Ngaga alikaririwa hivi karibuni akieleza kuwa SUA kwa sasa kinaendelea kufanya zaidi ya tafiti 200 za kilimo ili kukiwesha kilimo kuwa endelevu nchini.
Profesa Yunika alikuwa akizungumza wakati wa warsha kwa waandishi wa habari juu ya kilimo na lishe iliyofadhiliwa na Innovative Agriculture Research iAGRI SUA.
Alisema kwamba SUA ina nafasi kubwa ya kufanya mikakati inayopangwa na Serikali ukiwamo kuwezesha mpango wa Kilimo Kwanza kutekelezeka akieleza kwamba kuwapo kwa mpango wa kilimo endelevu kwa kutumia tafiti kutaleta manufaa kwa wakulima na taifa.
Alisema kuwa bado kuna upungufu unayotokana na kilimo kutokuwa katika mpangilio endelevu kufuatia tafiti hizo kutotumika.
Utafiti mwingine wa SUA
Mwaka 2012 kitengo cha Apopo katika chuo kikuu hicho kilibaini kuwa panya ni wanyama wenye uwezo mkubwa wa kunusa na kufanya kazi adimu kama za kutegua mabomu yaliyotegwa ardhini kwa umbali wa mrefu wa kipimo cha mita.
Utafiti huo ulianza kufanywa na raia wa Ubelgiji, Bart Weetgen, mwaka 1998 katika chuo Kikuu cha Antwerp nchini Ubelgiji.
Kwa mujibu wa kituo cha Apopo, Weetgen alianza kwa kuuchambua upekee wa panya, kabla ya kuanza kuwatumia kunusa mabomu.
“Weetgen aliona kuwa, panya wa porini aina ya rodent wanaopatikana zaidi Tanzania, wanaweza kubaini kirahisi mabomu yaliyofukiwa ardhini,”alieleza Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Apopo, Majenda Mhutila.
Kiongozi Mkuu wa Mafunzo kwa panya, SUA, Abdullah Mchomvu alieleza kuwa panya walionekana kufaa zaidi kufanya kazi hiyo kwa sababu ya maumbile yao.
cho kitatumika na watu katika kudhibiti panya,” alisisitiza .

Alisema kuwa umbile la panya pamoja na uzito wake humfanya asiweze kulipua mabomu ardhini mara anapoyabaini.
Lakini, pia panya walionekana kuwa na tabia ya kipekee ya kuhifadhi na kufukua.
“Kwa uasilia panya hukusanya mazao wakati wa mavuno, kisha kuyaficha katika mashimo shambani. Baadaye hutumia njia ya kunusa kuyapata mazao waliyoyaficha nyakati za ukame. Kwa maana hiyo, tulitumia sifa yake hiyo na kumtumia kubaini kwa kutumia harufu,” alisema Mchomvu.
Aliongeza kuwa panya walibainika kuwa na uwezo mkubwa wa kutumia pua zao kuliko kuona, kwani macho yao hayana nguvu nyakati za mchana.
“Ni nafuu zaidi kumtunza panya kuliko mbwa. Kwa mfano panya 200 huweza kukaa katika jengo moja. Panya wana uwezo wa kufuata zaidi vitendo, kuliko kutazama kinachofanywa na mwongozaji,”alisema akiongeza:
“Sifa hizi, ndizo zilizotumiwa na watafiti kumhakiki panya kuwa mteguaji bingwa wa mabomu kuliko binadamu au vifaa vya kiteknolojia.”
Wanavyoweza kutegua mabomu
Mchomvu aliweka wazi kuwa, ili panya aweze kuifanya kazi ya kutegua mabomu ni lazima apate mafunzo, ambayo humpitisha katika hatua tisa muhimu.
Aliitaja hatua ya kwanza kuwa ni kumfanya awe rafiki au kumjengea tabia za kumzoea mwanadamu.
Alibainisha kuwa mkufunzi wake hutakiwa kumfanya panya amzoee, kwa sauti na kwa harufu ili asimdhuru.

Chanzo: Mwananchi

0 comments: