LATEST POSTS

Showing posts with label CELEBRETY. Show all posts
Showing posts with label CELEBRETY. Show all posts

Thursday, June 25, 2015

Familia yasema maisha ya Bobbi Kristina wamemuachia Mungu

Maisha ya Bobbi Kristina Brown sasa yapo mikononi mwa Mungu na jamaa zake wanasubiri lolote lile kutokea.
Kauli hiyo imetolewa na mama yake mkubwa Pat Houston wakati wakimhamishia binti huyo katika hospitali ya wagonjwa mahututi.
 “Pamoja na kupewa huduma  bingwa za kitabibu katika hospitali mbalimbali hali ya Bobbi Kristina Brown imeendelea kuzorota.Kuanzia leo tumemuhamishia katika uangalizi wa wagonjwa mahututi.Tunamshukuru kila mmoja kwa sapoti mliyotupa na sala.sasa yuko katika mikono ya Mungu.”
Mtoto wa pekee wa Bobby Brown na Whitney Houston  amekuwa hospitalini toka Januari 31 baada ya kukutwa bafuni akiwa hajitambui.
Bibi yake Bobbi Kristina, Cissy Houston  amekuwa akitoa taarifa zinazokatisha tama akisema wazi kwamba hakuna matumaini ya uzima kwa mjukuu wake.