LATEST POSTS

Saturday, June 20, 2015

Wanafunzi wa Vyuo Vikuu wanaongoza kwa utoaji wa mimba kwa njia za kienyeji

Moses Mongo ambaye ni Mratibu wa Kanda ya Ziwa kutoka Taasisi ya Umoja wa Mataifa (UNA-TANZANIA) amesema wanafunzi wa Vyuo Vikuu wanaongoza kwa utoaji wa mimba kwa njia za kienyeji kwa kutumia mwarobaini na bluu ya kuweka kwenye nguo nyeupe.

Mongo alisema katika utafiti walioufanya mwaka 2014 katika Vyuo Vikuu vinne Kanda ya Ziwa wamebaini wanafunzi kutoa mimba kienyeji.

“Utafiti tuliofanya 2014 kwa kuzungumza na wanafunzi kila Chuo au Shule tumebaini wapo wanafunzi waliotoa mimba na wapo waliofariki kwa kutoa mimba lakini kwa kificho”—Moses Mongo.

Mongo alisema katika mazungumzo na wanafunzi hao walieleza kuwa suala la utoaji wa mimba ni la kawaida na matumizi ya kondomu huwa ni pale wanapoanza uhusiano kabla ya kuzoeana.

0 comments: