LATEST POSTS

Tuesday, January 28, 2014

Mafisadi Malawi mahakamani kesho

KESI dhidi ya maafisa wazamani wa serikali ya Malawi wanaodaiwa kuhusika na wizi wa mamilioni ya dola za Marekani kutoka hazina ya serikali inatarajiwa kuanza kesho.
Sakata hilo lilifichuliwa kufuatia jaribio la mauaji dhidi ya Mkurugenzi wa bajeti, Paul Mphwiyo, ambaye ameripotiwa alikuwa tayari kufichua kashfa kubwa zaidi .
Kwa mujibu wa BBC, inaelezwa kwamba hiyo ni kashfa kubwa zaidi kuwahi kutokea nchini Malawi.
Kashfa hiyo inayojulikana kama Cashgate imevuruga uhusiano mzuri ulioko kati ya Malawi na wafadhili huku raia wakikasirishwa na wizi huo wa mali ya umma.
Kashfa hiyo inaanzia katika eneo la kompyuta ambapo habari za siri kuhusu uwekaji fedha zimehifadhiwa.
Maafisa kadhaa wa Serikali wa mekuwa wakitumia udhaifu fulani katika mpango wa uhifadhi wa kompyuta hizo na kuiba mamilioni ya pesa kutoka hazina ya Serikali.
Inadaiwa kwamba huenda dola milioni 250 za Marekani ziliporwa kwa kuwalipa wafanyabiashara kimagendo kwa huduma ambazo hazikutolewa kwa Serikali.
Habari za uporaji huo wa mali ya umma zilifichuka wakati Mkurugenzi wa Bajeti katika Wizara ya Fedha, Paul Mphwiyo, alipopigwa risasi Septemba mwaka 2013.
Tukio hilo lilitekelezwa siku chache kabla ya mfanyakazi wa cheo cha chini serikalini alipopatikana na pesa taslimu ya dola 300,000 za Marekani katika buti la gari lake.
Pesa nyingi zaidi zilipatikana na kupokonywa wafanyakazi wa umma majumbani mwao katika buti za magari yao..

0 comments: