| Mtoto Anjela Rashid[4]amechomwa moto mikono yote miwili na baba yake mzazi baada ya kula finyango mbili za nyama zilizopikwa na Baba yake huyo | 
| Inasikitisha sana | 
| Mtoto amelala bila ya uwangali zi wa mtu yeyote yule | 
| Mtendaji wa mtaa huo Emmanuel Malema akihesabu mabati ili yauwze kwa ajili ya matibabu ya mtoto huyo | 
| Hapa ndipo anapo lala mtoto huyo | 
| Mabati yakitolewa ili yauzwe zipatikane fedha za matibabu ya mtoto huyo | 
Tukio 
la  pili limetokea machi 8 mwaka huu mtaa 
wa Kanda ya juu kata ya Iduda ambapo mtoto Anjela Rashid[4]ameunguzwa na moto 
mikono yote miwili  baada ya kula 
finyango mbili za nyama zilizopikwa na Baba yake.
Mama yake 
mzazi wa mtoto huyo hakuwepo wakati wa tukio hilo kutokana na kukimbia kwa 
mumewe Rashid Mwatiya[32]  ambapo 
amekimbilia Sumbawanga Mkoani Rukwa majuma mawili yaliyopita ili kuwepa vipigo 
vya mara kwa mara alivyokuwa akipata.
Baada ya 
kutenda unyama huo Mwatiya alimfungia mtoto huyo ndani bila kumpatia matibabu 
yoyote na chakula kwa hofu ya kukamatwa kutokana na majeraha makubwa mikononi 
hali inayomfanya mtoto kushindwa kula chakula kwa kutumia 
mikono.
Kutokana 
na vidonda kutopatiwa matibabu vidole vimeanza kuoza na kutokana na maumivu 
makali mtoto amekuwa akilia mara kwa mara ndipo kilio hicho kilibainishwa na 
Balozi Shaban Tolinga ambaye alitoa taarifa kwa Mwenyekiti wa mtaa lakini 
hakuchukua hatua zozote huku mikono ya mtoto ikioza.
Hata hivyo 
Mtendaji wa mtaa huo Emmanuel Malema baada ya kupata taarifa ya ukatili huo 
aliamua kufuatilia akiwa na waandishi wa habari ambapo mtoto alikuwa amelala 
sebuleni bila uangalizi wowote na njaa hali ilyomlazimu Mtendaji kuchukua mabati 
manne kuyauza ili kumpatia matibabu na chakula na kuhakikisha mtuhumiwa 
anakamatwa na kufikishwa kwenye mkono wa sheria.
Kwa upande 
wake Afisa Ustawi wa Jamii Kata ya Iduda amesema vitendo vya kikatili katika 
Kata yake vimekuwa vikifumbiwa macho kwa hofu ya kujenga uadui kwa watu wanaotoa 
ushahidi.
Aidha 
Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa amesema vitendo vya kiatili havita vumiliwa hivyo 
wananchi watoe ushirikiano ili kukomesha vitendo hivyo ambavyo vimekithiri kwa 
siku za hivi karibuni.
Chanzo: Mbeya yetu
 
 






 
 
0 comments:
Post a Comment