| 
John Msumba[3]ambaye amekuwa akipigwa mara kwa mara na 
wakati wote kufungiwa ndani kwa kufuli pia kunyimwa chakula na shangazi 
yake  | 
| TUNAOMBA RADHI KWA PICHA HII KWANI HATUNA JINSI IMEBIDI TUONYESHE KILA SEHEMU YA MWILI YA MTOTO HUYU KWA MATESO ALIYOKUWA AKIPATA HATA KUKAA ANASHINDWA | 
| Mwanahawa Nassoro[32] mkazi wa mtaa wa Airport Kata ya Iyela. ndiye anaetuhumiwa kumtesa mtoto John Msumba | 
Licha ya Asasi mbalimbali za kijamii kama TAMWA, GBV,TGNP 
na Dawati la jinsia la Jeshi la Polisi kukemea vitendo vya ukatili dhidi ya 
wanawake na watoto Mkoani Mbeya bado vitendo hivyo vimeendelea 
kushamiri.
Katika matukio mawili yaliyotokea Jijini Mbeya hivi 
karibuni yamewakumba watoto wawili wa wakazi wa Kata za Iyela na Iduda ambao 
wamejeruhiwa vibaya kwa vipigo na kuchomwa moto na walezi 
wao.
Tukio la kwanza limemhusisha mtoto wa kiume aliyefahamika 
kwa jina la John Msumba[3]ambaye amekuwa akipigwa mara kwa mara na wakati wote 
kufungiwa ndani kwa kufuli pia kunyimwa chakula na shangazi yake aitwaye 
Mwanahawa Nassoro[32] mkazi wa mtaa wa Airport Kata ya 
Iyela.
Vitendo hivyo vimetokana na kudaiwa mtoto huyo kujisaidia 
hovyo hali iliyomletea usumbufu Mwanahawa ambapo mama yake hayupo na Baba mzazi 
aliyefahamika kwa jina la Sumba Dinda akiwa machimboni wilaya ya Chunya 
takribani miezi miwili iliyopita.
Sakata hilo lilibainika baada ya kutokea msiba mtaani 
hapo Machi 12 mwaka huu majira ya saa nne asubuhi mtoto huyo alipokuwa akilia 
majirani walisogea eneo la tukio na kukuta mlango umefungwa kwa kufuli hivyo 
kumlazimu Mjumbe wa mtaa Bi Rehema Mohammed kutoa taarifa kwa Mwenyekiti wa mtaa 
huo Enock Mwampagama.
Mwampagama alitoa taarifa kwa Mtendaji wa mtaa Henry 
Chaula ambapo walimkamata kwa mahojiano katika ofisi ya mtaa na baada ya maelezo 
walimpeleka kituo cha Polisi Mwanjelwa kwa hatua 
zaidi.
Uchunguzi umebaini kuwa mtoto huyo amekuwa akiteswa kwa 
muda mrefu ingawa majirani na mwenye nyumba aliyefahamika kwa jina la Ollen 
Kaguo hawakuweza kutoa taarifa ili kunusuru afya ya mtoto ambaye ameonekana kuwa 
na ukosefu wa chakula bora na mwili ukiwa umejaa majeraha makubwa.
Chanzo: Mbeya Yetu
 
 






 
 
0 comments:
Post a Comment