LATEST POSTS

Tuesday, March 11, 2014

Wachimbaji wadogo ‘walilia’ leseni

Zaidi ya wachimbaji wadogo wa dhahabu 7000 wilayani Nzega mkoani Tabora wameiomba Serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini kuwapatia leseni ya uchimbaji katika mgodi mdogo wa dhahabu wa Mwanshina, uliopo pembezoni mwa mgodi mkubwa wa dhahabu wa Resolute.
Wakizungumza na waandishi wa habari katika mgodi huo, waliomba Serikali iwapatie leseni hiyo licha ya kukiri kuvamia eneo hilo kutokana na kukabiliwa na shida za kimaisha.

Walisema kuwa walivamia eneo hilo bila kuambiwa na kiongozi yeyote kutokana na ugumu wa maisha ya kukidhi haja zao za msing.

Mkazi wa Kijiji cha Mwanshina, JIsena Masanja alisema walivamia eneo hilo lililopo pembezoni mwa mgodi mkubwa ambalo halifanyiwi kazi na wawekezaji hao na kuongeza kuwa watalinda mazingira ikiwamo kuimarisha usalama kwa wananchi.


0 comments: