LATEST POSTS

Monday, July 27, 2015

Dokta amfungia baba’ke ndani miaka 4!

Haya ni madai mazito! Pamoja na kukanusha kwa nguvu zote, bado dokta wa  upasuaji wa Hospitali ya Wilaya ya Temeke, Dar aliyetajwa kwa jina moja la Twalib, anadaiwa kumfungia ndani baba yake mzazi, Harub Fitina akimuweka pamoja na kuku na sungura huku akipata mateso ya kunyimwa chakula na huduma nyingine za kibinadamu kwa miaka minne sasa, Ijumaa Wikienda limeibua mazito.

Dokta (3) ….Akipewa chakula.

Akizungumza na gazeti hili huku akirekodiwa, shangazi wa daktari huyo anayeishi Tegeta Masaiti, Kulwa Pazi alisema kuwa, Twalib alimchukua baba yake kutoka nyumbani kwake, Bagamoyo mkoani Pwani mwaka 2011 kwa ajili ya matibabu baada ya kuanguka ghafla na kupooza upande mmoja.
Alidai kwamba, siku chache baada ya kuhamia nyumbani hapo walishangaa kuwa kila wakienda kutaka kumuona mgonjwa waliishia nje kwa kisingizio kuwa mgonjwa anapaswa atulie na asisumbuliwe.

Dokta (2)…Nyumba alimofungiwa.

Alidai kwamba, kama hiyo haitoshi, mke wa mgonjwa ambaye walitengana siku chache baada ya mumewe kuugua, Siasa Mloli aliyebaki Bagamoyo alidai kuwa alikosa mawasiliano na huduma ya watoto kutoka kwa mumewe kwa kipindi hicho cha miaka minne.
Akizungumza na gazeti hili, mke wa Harub alisema kuwa, mapema mwaka jana, mtoto wake ambaye ni mwanafunzi aliyetajwa kwa jina la Jafar alikwenda nyumbani kwa Twalib kuomba fedha za matumizi lakini jamaa huyo alimfukuza, kisa aligonga mlango kwa kutumia jiwe.

IMG_0047-001…Akiwa na wanafamilia

Mbali na shangazi na mke wa jamaa huyo, ndugu wengine walidai kwamba, mapema mwaka huu walisikia kutoka kwa majirani kuwa Twalib anamtesa Harub na kumfungia kwenye banda la sungura na kuku, lakini walipofika nyumbani hapo dokta aliwafukuza.

_MG_0009-001…Akiwa amelala kitandani.

“Baada ya hapo tulikwenda kwa mjumbe wa mtaa na kuripoti kuhusu hali hiyo. Tukampelekea Twalib barua ya wito lakini siku ya kikao hakutokea,” alisema Siasa.

Ijumaa Wikienda lilipofika eneo la tukio liliwashuhudia ndugu hao wakizuiwa kuingia na mlinzi wa nyumba hiyo licha ya kuwa na mjumbe wa serikali ya mtaa kwa madai kuwa Twalib hakuwepo na hataki mtu yeyote aingie ndani kwake.
Ndugu hao na mjumbe walilazimika kuingia ndani kwa nguvu ambapo walijikuta wakitokwa na machozi kwa hali waliyomkuta nayo Harub akiwa amedhoofu.
Waandishi wetu walimshuhudia mgonjwa huyo akiwa amelala kwenye chumba kichafu ambacho upande mmoja kilikuwa kimetengwa kwa waya na chumba chenye kuku na sungura.
Hata hivyo, mgonjwa huyo aliangua kilio na kutoa sauti kwa tabu huku akitumia lugha ya ishara na kusababisha mkewe na mama yake mzazi aliyejitambulisha kwa jina moja la Mwamvua naye aangue kilio.
Mwishowe ndugu hao walimchukua Harub hadi Kituo cha Polisi cha Wazo Hill ili kutoa taarifa na kupewa jalada WH/RB/6116/2015, TAARIFA kisha waliondoka naye kumpeleka nyumbani kwao Kunduchi.
Waandishi wetu walipokutana na daktari huyo na  kumbwagia tuhuma hizo, alikanusha vikali ambapo alisema shangazi zake wanamzushia mambo mengi kwa kuwa wanataka mali za baba yake.

0 comments: