LATEST POSTS

Tuesday, July 21, 2015

MAGUFULI AZOA WANACHAMA WAPYA MJI MDOGO WA MUGANZA WILAYANI CHATO, GEITA



   Mgombea Urais kwa chama cha Mapinduzi CCM, Dkt. John Pombe Magufuli akipokea kadi za Wanachama wa vyama mbalimbali vya upinzani na kujiunga na CCM, jana jioni katika viwanja vya Mji mdogo wa Muganza, wilayni Chato Mkoani Geita, Mh. Magufuli amezoa wanachama wapya waliorudisha kadi zao wapatao zaidi ya 150.
  Dkt. Magufuli akipokea kadi za Wanachama wa vyama mbalimbali vya upinzani na kujiunga na CCM. Mh. Magufuli yuko jimboni kwake Wilayani Chato kuwaaga na kuwashukuru Wananchi wake kwa kumpa ridhaa ya kuwaongoza kwa miaka 20 akiwa Mbunge.
   MKe wa Magufuli, Mama Janeth Magufuli akiwasalimia na kuwashukuru Wananchi wa mji huo kwa mapokezi mazuri na makubwa waliyoyapata wilayani humo.
  Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara), Ndugu Rajab Luhwavi akiwasalimia wanachama wa CCM pamoja na Wananchi waliofika kumlaki Dkt. Magufuli jana jioni.
   Mgombea Urais kwa chama cha Mapinduzi CCM,Dkt John Pombe Magufuli akiwapungia mkono pia na kuwashukuru Wananchi wake kwa kumpa ridhaa ya kuwaongoza kwa miaka 20 akiwa Mbunge wao. 
  Baadhi ya Wananchi wa Muganza wakishangilia kwa  furaha kubwa mara baada ya Dkt. Magufuli kujitambulisha kwao na pia kuwashukuru kwa kumpa ridhaa ya kuwaongoza kwa miaka 20 ya Ubunge ndani ya jimbo hilo.
Wananchi wa Muganza wakimsikiliza Dkt. Magufuli. 
  Baadhi ya Wananchi wa Muganza wakishangilia kwa  furaha kubwa mara baada ya ,Dkt. Magufuli kujitambulisha kwao na pia kuwashukuru kwa kumpa ridhaa ya kuwaongoza kwa miaka 20 ya Ubunge ndani ya jimbo hilo.
    ..Furaha ikitawala.
  Dkt. Magufuli akiwaaga na kuwashukuru Wananchi wake kwa kumpa ridhaa ya kuwaongoza kwa miaka 20 akiwa Mbunge wao.
  Mmoja wa Wafuasi wa chama cha Chadema Jumanne Majani akionekana kuwa na furaha ya kupitiliza mara baada kumuona Dkt. Magufuli, katika kijiji cha Kibehe alipokuwa akielekea Mji Mdogo wa Muganza kuwasalimia na kuwashukuru wananchi wa Mji huo.
  Mmoja wa Wafuasi wa chama cha Chadema Jumanne Majani akionekana kuwa na furaha ya kupitiliza mara baada kupewa ruhusa ya kusalimiana na Dkt. Magufuli, katika kijiji cha Kibehe.
Jumanne Majani alipopewa fursa ya kuzungumza chochote.
 Baadhi ya Wananchi wakiwa wameziba barabara wakitaka kumuona na kumsalimia Dkt. Magufuli ikiwemo pia kumpongeza kwa kuteuliwa kuipeperusha bendera ya CCM katika kuwania Uraisi kupitia chama hicho
  Wafuasi wa CCM wakishangilia mara baada ya kumuona Dkt Magufuli alipokuwa akipita kuwasalimia wananchi.
 Mmoja wa Wafuasi wa CCM akishangilia mara baada ya kumuona Dkt Magufuli.
 
Chanzo: Global publishers

0 comments: