LATEST POSTS

Thursday, June 25, 2015

MJAMAICA KUTOA MAHALI YA HEKA 10 ZA BANGI ILI KIJANA WAKE AMUOE MTOTO WA OBAMA.

WANAUME WANAOMTAMANI KUMUOA BINTIYE RAIS OBAMA, MALIA OBAMA WANAZIDI KUONGEZEKA.

BAADA YA FELIX KIPRONOH WA KENYA NA MWENZAKE KUTOKA HUKO HUKO KENYA KUJITOKEZA NA NG’OMBE KADHAA KAMA MAHARI YA KUTAKA KUMUOA MALIA, JANA MZAZI MMOJA KUTOKA JAMAICA AMEJITOKEZA PIA NA MAHARI KWA AJILI YA KUMNASA MALIA OBAMA AWE MKE WA KIJANA WAKE.

MAHARI ILIYOTOLEWA MARA HII KUTOKA JAMAICA, SIO YA KAWAIDA MZAZI HUYO KWA JINA ROY CHAMBERS, AMEISHANGAZA DUNIA KWA KUTOA EKARI 10 ZA BANGI KAMA MAHARI KWA FAMILIA YA WHITE HOUSE KWA AJILI YA KUMPOSA MREMBO MALIA OBAMA KAMA MKE WA KIJANA WAKE.
MALIA OBAMA

“ NILIJARIBU KUMPATA OBAMA AKIWA HAPA JAMAICA WIKI CHACHE ZILIZOPITA LAKINI WALINZI WAKE WALINIZUIA, NIMEMTUMIA BARUA PEPE  NA NADHANI ATANIPA MREJESHO HIVI KARIBUNI”, CHAMBERS AMESEMA KATIKA MTANDAO WAKE.

“ SHAMBA LANGU LINA THAMANI KUBWA SANA KWANGU NA JAMAICA KWA JUMLA LAKINI KWA KUWA KIJANA WANGU ANAMPENDA MALIA OBAMA, NIKO RADHI KULITOA SHAMBA HILO KWA OBAMA ILI KIJANA WAKE AMUOE MREMBO HUYO” AMESEMA CHAMBERS.

0 comments: