LATEST POSTS

Sunday, May 18, 2014

PICHA ZA ZIARA YA ABRAHAM KINANA MJINI TABORA NA TIMU YAKE

Katibu Mkuu wa CCM, Kinana na timu walipokuwa wakiwasili kwenye Mkutano wa hadhara.

Baadhi ya Viongozi mbalimbali walioshiriki kwenye mkutano huo wa Hadhara.


Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akihutubia katika mkutano wa hadhara katika Uwanja wa Stendi Kuu ya Zamani mjini Tabora, baada ya kumaliza ziara yake ya siku 11 katika mkoa huo. Ziara ambayo imemchukua katika wilaya zote, kata na baadhi ya vijiji kwa ajili ya kuimarisha uhai wa chama, kukagua, kuhimiza na kusukuma miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwa kufuata Ilani ya Uchaguzi ya CCM, kukagua maandalizi ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa pamoja na kusikiliza kero za wananchi na kuzitafutia ufumbuzi.




Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye na Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Fatma Mwassa wakipata pia mlo kwa Mama Lishe.

Mbunge wa Jimbo la Tabora, Aden Rage (kushoto) akiungana na Kinana kula chakula kwa mama Lishe mjini Tabora leo kabla ya kuelekea kwenye mkutano wa hadhara.


Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye akihutubia katika mkutano wa hadhara wa CCM, Mjini Tabora leo, ambapo aliwafananisha UKAWA na Boko Haramu kwa jinsi wanavyowachonganisha wananchi kwa maneno ya kilaghai huku wakiwatukana waasisi wa taifa, kitendo ambacho alidai kinaweza kusababisha vurugu nchini


Mbunge wa Jimbo la Sikonge, Said Nkumba akihutubia katika mkutano huo.

0 comments: