LATEST POSTS

Saturday, July 4, 2015

Unatumia Nokia XL na unapata shida kudownload Whatsaap? Ufumbuzi huu hapa.

kizuri kula na wenzako.
Nilipopata simu ya Nokia Xl baada ya ile ya aina ya Samsung niliyokua nikiitumia awali tena nikiwa nimeetumia ndani ya kipindi kifupi sana toka nilipoinunua ( kama miezi mitano hivi), nilichanganyikiwa sana hasa kwa kukumbuka pesa yangu niliyotoa kununua simu ile aina ya samsung iliyonizimikia ghafla kama mshumaa. Nilijuta nikaona bora ile hela ningenunulia walao mifuko ya simenti nikafanyia kitu cha maana.
Mungu si Athumani, nilidunduliza pesa nikafanikiwa kununua simu nyingine aina ya Nokia Xl. Sasa nilikuja kupata shida sana kupata application ya Whatasaap kwenye simu hii. Nilihangaika sana lakini hatimaye nikapata msamaria mwema ambaye naye anatumia Nokia Xl. Nilipomuuliza kama katika simu yake hiyo anatumia whatsaap, alinijibu ndio. Nikapatwa na shauku ya kujua alifanyaje maana mie nilihangaika mno na kushirikisha wadau kadhaa ikiwepo na kugugle lkn ilinishindikana. Alinipa jibu rahisi sana, kwamba download kitu kitu kinachoitwa 1 Mobile Market kisha download whatsaap kupitia application hiyo. Nilipojaribu, ndani ya dakika kumi tu, kitu cha whatsaap kikawa hewani. Nilichekeleaje. Si mnajua tena whatsaap ndio mpango mzima siku hizi. Kama simu haina whatsaap ya kazi gani? Maana siku hizi tukienda dukani kununua simu cha kwanza hua tunauliza hivi, "Eti kaka/dada, hii simu ina whatsaap?". Sasa unainunua halafu unafika nyumbani, whatsaap hamna. Weee!Unachanganyikiwaje. Tafadhali, jaribuni hii kitu then mkifanikiwa mrudi hapa kutoa ushuhuda.

Nawapedeni sana fans wangu.

Teddy Chacha.

0 comments: