LATEST POSTS

Thursday, December 26, 2013

Maiti yabambwa na dawa za kulevya

Kamanda wa Polisi Mkoani Morogoro,Faustine Shilogile akizungumza na wanahabari (hawapo pichani).
Hizi ndio baadhi ya Pipi zilitolewa tumboni mwa Marehemu Khalid Kitala. …
Baadhi ya Makachero wa Polisi wakijadiliana jambo baada ya kuona Mwili huo.
Jeshi la Polisi mkoani Morogoro limefanikiwa kukamata gari dogo aina ya Toyota Spacio likiwa limebeba mwili wa mtu aliefari ambaye alitambulikwa kwa Jila la Khalid Kitala (47) na kukutwa na kete kadhaa za Madawa ya Kulevywa tumboni.
 

 JESHI la Polisi mkoani Morogoro limenasa kete 24 za dawa za kulevya kwenye mwili wa marehemu Khalid Abdul Kitala (47) mkazi jijini Dar es Salaam.
Mwili wa marehemu Kitala aliyekuwa akiishi Kariakoo, Mtaa wa Kongo, ulikuwa ukisafirishwa kutoka Mbeya kuelekea jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Faustin Shilogile, tukio hilo lilitokea juzi usiku katika mizani ya magari makubwa iliyopo Mikumi wilayani Kilosa.
“Baada ya taarifa za siri kutoka kwa wasamaria wema kuwa kuna gari dogo kutoka wilayani Mbozi baadae lilitambulika kuwa ni aina ya Spacio T 887 BSW limebeba mwili wa marehemu wenye dawa za kulevya, tukaweka mitego sehemu mbalimali na kulinasa Mikumi,” alisema Shilogile.
Alisema gari hilo lilikuwa likiendeshwa kwa kupokezana na Teddy Esco (27), mkazi wa Mtaa wa Mwaka, Tuduma, Wilaya ya Momba mkoani Mbeya na Lucas Atubonekisye Swila (32) wa Mtaa wa Songea wilayani Momba, lilikuwa na abiria aliyetambulika kwa jina la Jumbe Hamad Mbano (36), mfanyabiashara wa Kariakoo, Mtaa wa Jangwani jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa Shilogile, taarifa za uchunguzi za awali baada ya kukamatwa kwa gari hilo zilikutwa kete saba ndani ya gari zilizofanya jumla ya kete 24 katika tukio hilo na marehemu alikuwa mfanyabiashara katika soko la Kariakoo-Kongo jijini Dar es Salaam.
Naye Mganga Mkuu wa hospitali ya Rufaa Morogoro, Ritha Lyamuya alisema baada ya marehemu kufanyiwa uchunguzi zilitolewa kete 17 zinazohisiwa kuwa za dawa za kulevya.
Alisema mwili wa marehemu umehifadhiwa kwenye chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali hiyo kwa taratibu nyingine za kisheria kabla haujaruhusiwa kuzikwa.
Chanzo: Tanzania Daima and GPL

0 comments: