LATEST POSTS

Friday, January 24, 2014

Diamond atimiza ahadi

 
Diamond atimiza ahadi ya kusomesha watoto 

HATIMAYE mkali wa muziki wa kizazi kipya nchini, Nassib Abdul ‘Diamond Platinum’ ametimiza ahadi ya kuwasomesha watoto ambao walishinda shindano la kucheza mtindo wake wa ‘Ngololo’ katika sherehe alizoziandaa maalumu kwenye viwanja vya Leaders jijini Dar es Salaam, Desemba 25, mwaka jana.

Diamond aliandaa shoo hiyo ili kuwakutanisha watoto kwa pamoja na kuwashindanisha kucheza wimbo wake wa ‘My Number One’ ambao unafanya vizuri katika ‘game’ na kuwaahidi kuwasomesha watoto zaidi ya watano ambao walicheza vizuri wimbo huo.
Diamond kupitia mtandao wake wa ‘This is Diamond’, ameweka picha ambazo zinaonyesha yupo shuleni akiwa na watoto pamoja na wazazi wao wakiwaandikisha katika Shule ya East Africa International iliyopo Mikocheni jijini Dar es Salaam.
“Nilipanga kuwapeleka shule watoto waliocheza vizuri na nilitaka wapate elimu iliyo bora zaidi, nilikaa na uongozi wangu na kutafiti ni shule gani ambayo itakidhi mahitaji ya watoto wale, yenye mazingira mazuri ya kujisomea na kucheza, namshukuru sana Mkuu wa Shule hiyo, Bi. Mercy Githirua, kwa kutupokea vizuri,” aliandika msanii huyo.
Diamond ni kati ya wasanii wanaofanya vizuri katika tasnia ya muziki wa kizazi kipya, kutokana na ubora wa kazi zake ambazo zinakubalika katika jamii inayomzunguka.

0 comments: