LATEST POSTS

Saturday, July 26, 2014

TCAA wamtwika zigo Mwakyembe

Dar es Salaam. Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe jana alijikuta akitwishwa masuala mazito kutoka kwa wafanyakazi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA), ambao walibainisha changamoto nyingi zinazowarudisha nyuma kutekeleza majukumu yao.
Asilimia kubwa ya changamoto hizo zimesababishwa na urasimu na migongano iliyopo katika idara za Serikali ambazo kwa mujibu wafanyakazi hao, zimefanya hadhi ya sekta ya usafiri wa anga ishuke.
Baadhi ya mambo hayo ni kucheleweshwa kwa rasimu ya sheria ya usimamizi wa utafutaji na uokoaji katika ajali za ndege bungeni ambayo haijafanyiwa kazi kwa takriban miaka 10 jambo ambalo limeifanya TCAA ishindwe kutimiza masharti ya kimataifa.
Mengine ni kuhamishwa kwa mpango mkuu wa usafiri wa anga nchini (Civil Aviation Master Plan) kwenda kwa Mamlaka ya Viwanja wa Ndege (TAA) kutoka TCAA kinyume na taratibu za Shirika la Kimataifa la Usafiri wa Anga (Icao) na upungufu wa mitambo ya kisasa kusimamia shughuli za anga.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TCAA, Charles Chacha alisema mamlaka yake kwa sasa ina changamoto lukuki ukiwemo uhaba wa wataalamu wa ukaguzi.

0 comments: