LATEST POSTS

Wednesday, August 5, 2015

MH370:Uchunguzi wa kina waanza Ufaransa

 

Watalamu kutoka Ufaransa, Malaysia na Australia wameanza kuchunguza mabaki ya bawa la ndege iliyopatikana juma lililopita likiwa limesombwa hadi ufukweni na maji ya bahari Hindi katika kisiwa cha Re-Union karibu na Madagascar.
Nia hasa ni kubaini iwapo mabawa hayo ni sehemu ya mabaki ya ile ndege ya Malaysia ya MH370, iliyotoweka.

Inaaminika kuwa mabaki hayo ni kipande cha bawa la ndege hiyo ya MH370
Mabaki hayo yamehifadhiwa katika kambi ya jeshi iliyoko katika mji wa Toulouse.

Wataalamu hao watachukua alama za rangi na alama nyingine yeyote ile itakayowasaidia katika utambuzi wa ndege hiyo.


Sehemu iliyoshikana na ndege pia inachunguzwa ili kujua ilimeguka kutoka wapi.

Ndege hiyo ya MH370, ilitoweka angani mwezi Machi mwaka jana ikiwa na abiria 239 na wahudumu wa ndege.

chanzo: BBC SWAHILI

0 comments: